Friday, November 30, 2012

Ushahidi mpya wa mauaji ya Mau Mau


Baadhi ya wapiganaji wa Mau Mau waliodhulumiwa na wakoloni wa Uingereza
Stakabadhi za Serikali zilizotolewa huko Uingereza zinaonyesha kwa ukamilifu namna wafungwa wengi waliuawa wakati wa uasi wa kundi la Mau Mau nchini Kenya.
Wakenya kumi na mmoja walipigwa na walinzi hadi kufa katika kambi walikozuiliwa ya Hola huku wengine wakijeruhiwa mwaka 1959.
Mzee moja manusura wa mauaji hayo kwa sasa ameshtaki serikali ya Uingereza akidai aliteswa.
Stakabadhi hizo zinaonyesha mkutano uliongozwa na aliyekuwa gavana wa Kenya na maafisa wakuu wa magereza kumbukumbu zinazoonyesha kuwa maafisa hao walikiuka haki za binadamu lakini hawakufunguliwa mashtaka.

No comments: