Monday, November 26, 2012

HABARI NA PICHA ZAIDI MAZISHI YA ASKOFU PASCAL KIKOTI HUKO MPANDA


Maskofu wakipita kuaaga mwili wa marehemu Askofu Pascal Kikoti wa jimbo la mpanda aliyefariki hivi karibuni katika hospitalia ya Bungando jijini Mwanza alikokuwa akitibiwa.
(Picha zote na Kibada Kibada Fullshangwe- Katavi)
Waziri mkuu Pinda akiwa miongoni mwa waumini wa kanisa katoliki jimbo la Mpanda katika ibada ya mazishi ya Askofu Pascal Kikoti misa katika iliyofanyika leo jumamosi septemba mosi 2012.Askofu mkuu jimbo kuu  la Dar es salaam Kadnari Pollycarp Pengo akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Askofu Kikoti.Waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda akiweka shada la maua kwenye kaburi la askofu Kikoti katika mazishi yaliyofnaya kanisa la Mt. Maria Emakulata  jimbo la Mpanda.
Na Kibada Kibada Fullshangwe-Mpanda
Waziri mkuu Mizengo Pinda leo ameongoza mamia ya waombolezaji wa jimbo katoliki la mpanda kuuaga mwili wa  marehemu Askofu wa jimbo la Mpanda Askofu Pascal Kikoti aliyefairiki dunia kwa shinikizo la damu.
Akitoa salaamu  za serikali waziri mkuu Pinda amesema kanisa limepoteza nguzo kubwa na tegemeo la kanisa na jamii kwa kuwaalikuwa mtu wa pekee kutokana na juhudi zake alizokuwa akizionesha za kuleta maendeleo katika jimbo la mpanda na jamii ya watanzania kwa ujumla hususani waumini wa kanisa la katoliki jimbo la mpanda na Tanzania kwa ujumla.
Waziri mkuu Pinda alisema Mhashamu Askofu kikoti alifanya kipindi cha maisha yake ya uinjilisti hapo jimboni na kutoa mchango  wake mkubwa ambao uligusa jamii nzima na siyo tu katika kutoa huduma za kiroho, balipia huduma za kijamii zilizolenga kuleta maendeleo kwa wananchi katika jimbo la mpanda na nchini kwa ujumla
nyota ya Askofu wa jimbo katoliki la mpanda Mhashamu Pascal Kikoti imezimika leo alipohitimisha safari yake hapa duniani pale kwenye kanisa katoliki na kuacha vilio simanzi na majonzi mazito kwa wakazi wa mpanda na waumini wote wa wilaya ya mpanda mkoa wa katavi kwa ujumla.
Mhashamu baba Askofu Kikoti ametutoka hiyo ni kauli yake waziri mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa wakati akitoa salaamu kwa niaba ya serikali mara baada ya kumalizika kwa ibada ya maziko iliyoongozwa na kadinari Polcapy Pengo askofu mkuu wa jimbo kuu la Dar es salaam.
.
“Mimi binafsi nimefanya kazi kwa karibu sana na Mhashamu Askofu Kikoti, tangu alipowekwa wakfu na kusimikwa kuwa Askofu wa Jimbo la mpanda mwaka 2001, na hata kabla.nilifairijika sana na uongozi wake, maono yake na shauku yake ya kutoa huduma za kiroho na za kijamii kwa jumla ,hivyo basi ni dhahiri kwamba kifo hiki ni pigo kubwa siyo kwangu, au kwa waumini wa kanisa katoliki, au wanampanda tu, bali wananchi wote nchini kwa jumla” alisema waziri mkuu Pinda.
“Mhashamu Askofi Kikoti ametutoka akiwa na umri mdogo sana wa kiuchungaji wa miaka 55,utumishi  wake ulitukuka bado ulikuwa unahitajika sana, kwa maneno mengine ,badoangeendelea kutoautumishi kwa miaka mingine mingi zaidi,kabla ya kifo chake alikuwa na malengo mengi mazuri yakiwemo yakufungua seminari ndogo ya jimbo,kujenga kituochakiuchungaji na jamii na kupanua shule ya sekondari ya mtakatifu Maria ya hapa Mpanda,lakini mungu ameamua amuchukemapema “alisema  waziri mkuu Pinda.
Alisema anatambua machungu waliyowapata wanampanda kwa kupoteza kiongozi nguzo ya jimbo la mpanda ,kikubwa ni kumunzi kwa kuendeleza yale mazuri aliyoaanza marehemu Kikoti na kwa njia hiyo watakuwa wameendeleza ile kauli mbiu yake inayosema kwamba “katika imani na upendo “alisema panda hiyo ilikuwa kauli mbiu ya mhashamu Askofu Kikoti.
Hata hivyo waziri mkuu Pinda alisema mungu atawaongoza  katika kumpata mrithi wake ambaye ataendeleza kauli mbiu hiyo pamoja na kukamilisha malengo aliyokuwa nayo.muhimu nni kumwombea kwa mwenyezi mungu aipumzishe Rohpo ya Marehemu mahali pema peponi.
Awali Akisoma salama za rambirambi zilizotumwa na mhe,Rais Jakaya Kikwete kwa Rais wa baraza la maaskofu Tanzania Askofu Tarcirius Ngalalekumtwa salaamu zilizosomwa na katibu wa maaskofu  Padri Anton Makunde mhe, Rais katika salamu zake alisema kanisa limpoteza mtu muhimu ambaye utumishi wake kwa kanisa taifa na jamii kwa umla bado vilikuwa vinahitajika sana.
Alisema yale yote mema aliyoyafanya Askofu Kikoti  ni vyema yaendelezwe na kuenzi ili kumuenzi Mhashamu Askofu Kikoti na wao kamaviongozi wa Taifa wataendelea kuyaenzi.
Akisoma wasifu wa marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Tabora Paulo Ruzoka alisema marehe Kikoti alizali wilayani Kilolo katiaka kijiji cha —-na kusoma  elimu ya msingi mkoani iringa kasha kujiunga na seminari ya  mafinga, Tungamo,Peramiho,kiparapala, Nyegezi  kasha kwenda roma italia kwa ajili ya kusomea historia ya mababa wa kanisa na aliporejea alikuwa akifundisha seminari ya peramiho hadi alipoteuliwa kuwa Askofu wa kwa jimbo la mpanda hadi kifo cha alikuwa askofu wajimbo lampanda ambapo ametumikia miaka kumia na moja.
Misa  ya maziko imeongozwa na kadri Pengo  ambapo katika misha hiyo Askofu wa Jimbo la Sumbawanga Damian Kyarusi aliteuliwa na Baba mtatifu Benidikto wa kumi na sita kuwa mwangalizi wa jimbo la mpanda hadi hapo taratibu nyingine zitakapofanyika.
Kwa upande wake Askofu Kyarusi naye alimteua Padri Patrick Kasomo kuwa msaidizi wake kwaambapo awali Padri Kasomo alikuwa msaidizi wa Askofu Kikoti aliyefariki dunia.kuteuliwa kwa Askofu Kyarusi ni kutokana na kuwa awali alikuwa akitumika hadi mpanda kwabla haijapewa hadhi ya kuwa jimbo.uteuzi huoulitamuka na Balozi wa Papa hapa nchini Askofu Franssco  Padino.

No comments: