Monday, November 26, 2012

Al-Shabaab watolewa Beled Hawo Somalia

 

Taarifa kutoka Somalia zinaeleza kuwa watu kama 12 wameuwawa katika mapigano baina ya jeshi la serikali na wapiganaji wa Al Shabaab karibu na mpaka wa Kenya.
Wapiganaji wa al-Shabaab
Kamanda wa eneo hilo alisema al-Shabaab kwa muda mfupi walidhibiti mji wa Beled Hawo, ulio mpakani, kabla ya kushambuliwa na kutimuliwa.
Kila upande unadai kuwa upande wa pili umepata hasara kubwa zaidi.
Al Shabaab bado wanadhibiti maeneo mengi ya kusini na kati mwa Somalia ingawa wamekimbizwa Mogadishu awali mwaka huu.


Mabomu yaripuliwa kambini Kaduna

 

Jeshi la Nigeria linasema kuwa mabomu yaliyotegwa kwenye magari mawili yameripuliwa ndani ya kambi ya karibu na mji wa Kaduna, kaskazini mwa nchi.
Kanisa la Kaduna liloshambuliwa mwezi Oktoba
Watu kama 11 waliuwawa na 30 kujeruhiwa.
Mshambuliaji wa kwanza alikuwa kwenye basi lilojaa mabomu na aligonga kanisa wakati ibada ya Jumapili ikimalizika.
Dakika 10 baadae gari lilotegwa bomu liliripuka nje ya kanisa.
Jeshi la Nigeria limelaumu kundi la wapiganaji wa Boko Haram.
Msemaji wa jeshi alisema mashambulio hayo ndani ya kambi ilioko Jaji, yatia aibu.
Boko Haram inapigana kuipindua serikali ya Nigeria, ili kuweka sheria kali za Kiislamu.

No comments: