Wednesday, November 28, 2012

''Katu hatuondoki Goma'' wasema M23



Waasi wa M23 wamewalazimisha watu kutoroka mji wa Goma
Kiongozi wa waasi wa M23 ambao wiki jana waliuteka mji wa Goma Mashariki mwa DRC, wanasema katu hawataondoka Goma hadi serikali itakapotimiza matakwa yao.
Kiongozi wa kundi hilo, Jean-Marie Runiga alisema kuwa wapiganaji wake wataondoka mara moja ikiwa Rais Joseph Kabila, ataitikia matakwa yao ambayo ni pamoja na kuivunja tume ya uchaguzi.
Serikali ya Congo hata hivyo imepuuza matakwa hayo kama ya kipuuzi.
Uganda ambayo imekuwa ikipatanisha pande hizo mbili kwenye mkutano mjini Kampala, awali ilisema walikubali kuondoka Goma bila vikwazo.
Mnamo Jumamosi, serikali za nchi za Maziwa makuu ziliwapatia waasi hao makataa ya siku mbili kuondoka Goma.

No comments: