Sunday, June 9, 2013

TAZAMA JINSI WASHINDI WA TUZO HIZO ZA KILIMANJARO TANZANIA MUSIC AWARDS 2013. WALIVYOJINYAKULIA TUZO HUKU KALA JEREMIAH NA OMMY DIMPOZI WAKIONGOZA

MTUNZI BORA WA MASHAHIRI HIP HOP-KALA JEREMIAH
WIMBO BORA WA KUSHIRIKIANA;OMMY DIMPOZ ft VANESSA-ME AND YOU
MTUNZI BORA WA MASHAHIRI -BENDI; CHARLS BABA


                    WIMBO BORA WA RNB; RAMA DEE ft MAPACHA-KUWA NA SUBIRA

                                KIKUNDI BORA CHA TAARABU-JAHAZI MODERN TAARAB

MTUNZI BORA WA TAARABU-THABIT ABDUL

WIMBO BORA WA TAARABU;KHADIJA KOPA-MJINI CHUO KIKUU

MTAYARISHAJI WA WIMBO WA MWAKA KWA TAARABU-ENRICO

                                       MSANII BORA WA KIKE -TAARBU; ISHA MASHAUZI


                                       MTUNZI BORA WA MASHAHIRI BONGO FLAVA-BEN POL



                             MSANII BORA WA KIUME BONGO FLAVA-DIAMOND

                                    MSANII BORA WA KIKE BONGO FLAVA-RECHO


KIKUNDI BORA CHA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA-JAMBO SQUAD
MTAYARISHAJI CHIPUKIZI WA MWAKA-MENSEN SELECTA
MSANII BORA WA KIKE-BENDI ;LUIZA MBUTU
WIMBO BORA WA ZOUK; AMINI -NI WEWE





Mwaka huu umekuwa mwaka mzuri zaidi kimuziki kwa msanii toka rock City Mwanza Kala Jeremiaha ambae maombi yake kwa ‘Dear God’ yamesikika na amepata majibu kwa njia ya kipekee na wimbo wake ‘Dear God’ umeweza kuchukua tuzo tatu katika Kilimanjaro Music Awards 2013.  
 
Kala Jeremiah ametumia mkuki mmoja kunasa ‘swala’ wake watatu muhimu mwaka huu, Dear God imeweza kumpa nafasi kubwa na kushinda tuzo katika kipengele cha wimbo bora wa Hip Hop.



Nguvu ya wimbo huo hapana shaka ndiyo imemuwezesha pia kuondoka na tuzo ya msanii bora wa Hip Hop na Mtunzi bora wa mashairi ya Hip Hop.

Kala aliweza kuwapenya wasanii wazito kama Fid Q, Joh Makini, Mwana FA, Profesa Jay na mdogo wake katika game Stamina wa Moro Town waliokutana nae katika vipengele vya Hip Hop.

Wimbo huu ulitengenezwa na mtayarishaji chipukizi Dee Classic ambae pia alikuwa anawania tuzo katika kipengele cha mtayarishaji chipukizi wa Mwaka lakini hakuweza kushinda tuzo hiyo ambayo ilienda kwa Mesen Selector.
Msanii mwingine wa bongo fleva aliyeng’ara katika tuzo hizo ni Ommy Dimpoz ambae pia aliondoka na Tuzo tatu, ambazo ni Video bora ya wimbo bora ya mwaka, wimbo bora wa Bongo Pop ‘Me and You’ akiwa na Vannessa Mdee ambao pia uliwapa tuzo ya wimbo bora wa kushirikishwa/kushirikiana.

Wasanii na watayarishaji wa muziki wa bongo fleva ambao kwa mara ya kwanza wameweza kujishindia tuzo za Kili ni pamoja na kundi la Jambo Squared toka Arusha (Kundi bora la muziki wa kizazi kipya), Rama Dee ‘Kinega’ (Wimbo bora wa RnB ‘Kuwa na subira).

Wengine ni Amini (Wimbo bora wa Zouk Rhumba ‘Ni wewe’), Recho (Msanii bora wa kike Bongo fleva), na Nay wa Mitego (Wimbo bora wa Hip Hop ‘Nasema Nao’). Mesen Selecter (Mtayarishaji chipukizi wa Mwaka), Ali Nipishe (Msanii bora anaechipukia).

Tuzo hizo zimeshuhudiwa huku mfalme na malkia wa muziki wa kibongo wakitangazwa kuwa Lady Jay Dee ‘Anaconda’ (Msanii bora wa Kike) na Diamond Platinumz (Msanii bora wa kiume).

No comments: