Sunday, June 2, 2013

INASIKITISHA:HUYU NDIYE MWANAMKE ANAYEISHI KAMA MKIMBIZI BAADA YA KUNUSURIKA KUCHINJWA.SOMA ZAIDI HAPA


Mwanamke Mery Mbosa anayeishi kama mkimbizi baada ya kunusurika mara kadhaa kuchinjwa na mtalaka wake.
------------------------------------------------------------

Na Gustav Chahe, Iringa
MAMA mmoja mkazi wa Itunundu – Pawaga katika Mkoa wa Iringa Mery Mbosa anaishi kama digidigi baada ya kunusurika mara kadhaa kuchinjwa na mtalaka wake na kulazimika kuhama kijiji kwa ajili ya kunusuru maisha.
Akiongea na mtandao huu jana, Bi Mbosa alisema maisha yake yapo hatarini kutokana na kuvamiwa na mtalaka wake mara kadhaa akiwa nyumbani na kumuumiza.
Alisema alilazimika kutalakiana baada ya mwanamume huyo kuwa mkorofi kiasi cha kupigwa, kutokuwa huru kutumia mazao ambayo walilima wote na hata kutokuwa huru kuongea na watu hata kama ni ndugu zake kwa madai kuwa ni wivu wa kimapenzi.
Alisema mtalaka wake amegeuka kuwa mnyama na kufika nyumbani kwake usiku wa manane na pindi anapokuta mlango umefungwa huanza kurusha mawe madirishani huku akitaka kuvunja mlango ili kuingia kumdhuru.

No comments: