Sunday, January 6, 2013

TAARIFA KUHUSU JAY JAY OKOCHA KUFILISIKA

.
Taarifa kutoka kwenye magazeti manne makubwa ya Nigeria zimeripoti kwamba mchezaji maarufu na wa siku nyingi nchini humo Jay Jay Okocha anazidi kufilisika kila siku na sasa anafanya muendelezo wa kuuza mali zake ambazo zilikua kitega uchumi kikubwa kwake.
Captain huyu wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria ambae pia alizichezea Bolton Wanderers and Hull City tayari mpaka sasa ameshaiuza club yake maarufu Nigeria iitwayo Club 10 ambayo ameiuza kwa Producer Don Jazzy ambae ni producer aliewatoa wengi akiwemo D’Banj, na sasa anafanya kazi na staa Tiwa Savage.
Akon ndani ya Club 10
Club 10 ni kiwanja maarufu sana kwenye mji wa Lagos ambapo kimehudhuriwa na mastaa kibao akiwemo Akon.
Baada ya kuiuza hiyo Club, sasa hivi anauza nyumba yake nyingine iko Akute, Ogun State ambapo mpaka sasa imeripotiwa kwamba midfield Maestro yuko tayari kufanya mazungumzo ya kuanzia N17 million.

No comments: