Saturday, July 19, 2014
MICHARAZO MITUPU: HII NDIYO RATIBA YA LIGI KUU YA ENGLAND 2014-2015
MICHARAZO MITUPU: HII NDIYO RATIBA YA LIGI KUU YA ENGLAND 2014-2015: KIPUTE cha Ligi Kuu ya England inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia Agosti 16 mwaka huu ambapo tayari Chama cha Soka cha nchini hiy...
Tuesday, July 1, 2014
Sunday, June 29, 2014
Saturday, June 21, 2014
MATUKIO NA VIJANA: ANGALIA PICHA ANACHOKIFANYA HUYU JAMAA NA MFALME W...
MATUKIO NA VIJANA: ANGALIA PICHA ANACHOKIFANYA HUYU JAMAA NA MFALME W...: He trusts lions enough to stick his arm in their mouth!
Tuesday, June 17, 2014
MATUKIO NA VIJANA: MPYA KABISA: NAFASI ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO ZA...
MATUKIO NA VIJANA: MPYA KABISA: NAFASI ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO ZA...: Nafasi za kujiunga na kidato cha nne mwaka 2014 kwa wanafunzi waliomaliza mwaka jana zimetangazwa rasmi muda huu jijini dare s sal...
Friday, June 13, 2014
Monday, June 9, 2014
MATUKIO NA VIJANA: KAULI YA SERIKALI BUNGENI KUHUSU PICHA CHAFU MTAND...
MATUKIO NA VIJANA: KAULI YA SERIKALI BUNGENI KUHUSU PICHA CHAFU MTAND...: Sakata la kusambaa picha zisizokuwa na maadili mitandaoni zikiwemo za watu maarufu hapa nchini leo limezungumziwa tena katika bunge la Tanz...
Thursday, June 5, 2014
Wednesday, April 30, 2014
ANGALIA PICHA ZA AJALI ILIYOUWA WATU 19 MKOANI SINGIDA WAKIWEPO POLISI 4
Wednesday, April 30, 2014
Basi hilo la kampuni ya Sumry hufanya safari zake
kati ya Kigoma na Dar-es-salaam. Dereva wa basi hilo alikimbia mara tu
na baada ya ajali hiyo na kulitekeleza basi hilo.
Watu 19 wa kijiji cha Utaho wilayani Ikungi wamepoteza maisha wakiwemo askari wanne wa jeshi la polisi, baada ya kugongwa na basi la Summry wakati wakiwa wana toa msaada wa kumpakia marehemu kwenye gari la polisi aliye gongwa na gari kubwa ambalo halikufahamika mara moja .Mwandishi wa habari wa ITV alifika na kuwakuta wasafiri walionusurika wakiwa katika kituo cha polisi cha Ikungi bila ya kujua hatima yao ya safari baada ya basi lao kuwakanyaga na kuuwa watu 19
Gari la
polisi likiwa limepakia maiti zaidi ya kumi zikipelekwa hospitali ya
mkoa wa singida kwa ajili ya kuhifadhiwa na kutambuliwa
PICHA ZOTE NA :Elisante Mkumbo-Singida
Moja
ya maiti ya ajali ya basi la sumry iliyo tokea katika kijiji cha
Utaho Wilayani Ikungi ikisubiri kupakiwa katika gari la polisi.
Baadhi ya miili ya wakazi wa kijiji cha Utaho wilaya ya Ikungi, waliogongwa na basi la Summry ikiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa wa Singida mjini humo.

Baadhi ya miili ya wakazi wa kijiji cha Utaho wilaya ya Ikungi, waliogongwa na basi la Summry ikiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa wa Singida mjini humo.
Saturday, March 8, 2014
HIZI NDIZO HOTEL 10 BORA ZAIDI DUNIANI...NI NZURI BALAA
1. Marina Bay Sands, Singapore

Mpaka kukamilisha kuijenga hoteli hii, bajeti ya dola bilioni 8 zilitumika.
2. Sheraton Huzhou Hot Spring Resort

3. Resorts World, Sentosa, Singapore

Dola bilioni 6.5 zilitumika kujenga hoteli hii na ndani kuna hoteli sita zinazojitegemea.
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
4. Mardan Palace, Lara, Antalya, Uturuki

Hoteli hii ilizinduliwa mwaka 2009, na uzinduzi wake ulikuwa mkubwa zaidi katika historia ya uzinduzi wa hoteli duniani.
5. City Of Dreams, Macau, China

Kama panavyoitwa, ‘Jiji la Ndoto’ hapa utakutana na hoteli 3 kubwa, Hard Rock Hotel, Grand Hyatt Macau, na Crown Towers.
6. The Venetian, Macau, China

Panahusu
mazungumzo ya casino, basi The Venetian, Macau ni baba lao. Ikijengwa
kwa dola bilioni 2.4, ilipomalizka ilikuwa na casino kubwa zaidi
duniani.
7. The Cosmopolitan, Las Vegas

Hii ni sehemu ambayo maceleb hujivinjari zaidi. Ilijengwa kwa gharama ya dola bilioni 4.9.
8. Emirates Palace, Abu Dhabi

Ujenzi wa kiota hiki ulitumia gharama ya dola bilioni 5 na kuifanya kuwa miongoni mwa majengo aghali zaidi.
9. Burj Al Arab, Dubai

Ukiitaja
‘Dubai’, kulitaja jina Burj Al Arab huwezi kuliepuka. Ujenzi wake
ulitumia miaka sita kwa gharama ya dola milioni 650. Na ilipofunguliwa
mwaka 2000, jengo hili likawa refu kuliko majengo yote duniani.
10. Atlantis, The Palm, Dubai
Ujenzi wa jengo hili uligharimu dola bilioni 1.5
Tuesday, March 4, 2014
MAAJABU YA DUNIA ! MTOTO WA MIAKA 5 ALIYEBEBA UJAUZITO NA KUJIFUNGUA MTOTO WA KIUME NCHINI PERU.
LINA MEDINA
LINA AKIWA MJAMZITO.
LINA
AKIWA NA MTOTO NA MMOJA WA MADAKTARI WALIOMFANYIA UPASUAJI NA
KUJIFUNGUA MTOTO HUYO KATIKA KITANDA CHA WATOTO CHA MATAIRI MANNE.
LINA Medina aliyezaliwa tarehe 27 Sept. 1933, huko Ticrapo, mkoa wa Huancavelica, nchini Peru, anatajwa kua Mama mwenye umri mdogo kuwahi kutokea katika historia ya Ulimwengu.
Tarehe 14 Mei 1939 Lina akiwa na umri wa miaka 5 na miezi 7, alijifungua mtoto wa Kiume aliy
e mpa jina la Gerardo Medina.
Ilianzaje?
Mwanzoni mwa mwezi Machi 1939 wazazi wa Lina ~ Tiburelo Medina na Victoria Losea waliamua kumpeleka Hospitali baada ya kuona tumbo likiongezeka kupita kiasi.
Wazazi wa Lina walidhani huenda ana uvimbe tumboni, lakini madaktari waligundua kua alikua ana ujauzito wa miezi 7.
Dr. Gerardo Lozada aliamua kumpeleka Lina kwa wataalam zaidi nao wakathibitisha kua ni kweli alikua mja mzito.
Alizaaje ?.
Mwezi mmoja na nusu baada ya kupelekwa hospitali kwa mara ya kwanza, Lina alijifungua mtoto wa kiume kwa njia ya upasuaji, kutokana na njia yake ya uzazi kua ndogo.
Upasuaji ulifanywa na Dr. Lozada, Dr. Busalleu, na Dr. Colareta.
Alivunja Ungo lini?.
Dr. Edmundo Escomel alitoa ripoti kamili juu ya kesi ya Lina kupitia jarida maalum la maswala ya kiafya na matibabu liitwalo La Presse Médicale.
Ripoti hii ilibainisha kwamba Lina alianza kupata siku zake tangu akiwa na umri wa miezi 8, alitofautiana na ripoti ya awali iliyosema kua amekua akiona siku zake tangu alipokua na umri wa miaka 3.
Ripoti hii pia ilisema kua Lina alianza kuota maziwa akiwa na umri wa miaka 4, alipofikisha miaka 5 nyonga yake ilikua imesha tanuka.
Alizaa mtoto gani ?.
Mtoto alizaliwa na uzito wa kilo 2.7 na alipewa jina la daktari wake Gerardo.
Gerardo alilelewa akijua kwamba lina ni dada yake lakini alikuja kujua ukweli akiwa na umri wa miaka 10.
Gerardo aliendelea kukua akiwa mtoto mwenya afya njema lakini alifariki mwaka 1979 akiwa na miaka 40 kwa ugonjwa wa mifupa ujulikanao kwa jina la kitaalam la Bone marrow.
Nani Baba wa mtoto ?.
Lina hajawahi kumtaja baba wa mwanae wala mazingira yaliyopelekea yeye kupata mimba.
Dr. Escomel alipendekeza kwamba inawezekana hata Lina mwenyewe alikua hajui, na kusema kuwa hakutoa majibu yanayojitosheleza.
Tuhuma kwa baba mzazi:
Hata hivyo Baba mzazi wa Lina alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la Unyanyasaji wa kingono wa mtoto (Child Sexual Abuse) lakini aliachiwa baadae baada ya kukosekana ushahidi wa kutosheleza.
Na hivyo basi Baba halisi aliyempa mimba Lina hakuwahi kujulikana.
Maisha ya Lina baadae:
Miaka kadhaa baadae Lina aliolewa na Raúl Jurado ambaye mwaka 1972 walipata mtoto wa kiume.
Lina yupo hai mapaka sasa na anaishi maisha ya kimasikini huko Lima nchini Peru
UTAFITI !!!!: KUKOSA KIFUNGUA KINYWA ASUBUHI NI MOJA YA SABABU 5 ZA KUUDHURU UBONGO WA BINADAMU.
- Kukosa Kifungua Kinywa asubuhi
Watu wanaokosa kifungua kinywa asubuhi wanapata upungufu wa kiwango cha sukari kwenye damu. Hii husababisha upungufu wa madini (nutrients) kwenye ubongo na hatimaye ubongo hudhoofika. - Kula kupita kiasi:
Inasababisha kukaza kwa misuli au mishipa ya Ubongo na hatimaye hupelekea kudhoofika kwa mfumo wa fahamu. - Kuvuta Sigara:
Kwenye sigara kuna kitu kinaitwa Nikotini ambayo ndani yake kuna chembechembe ambazo zina sababisha makunyanzi kwenye ubongo na kisha kudhoofu. - Kutumia Sukari nyingi:
Matumizi ya sukari nyingi husababisha matatizo katika mfumo wa unyonyaji wa Protini na Madini joto mwilini na kusababisha ugonjwa wa Utapiamlo ambao pia huingilia mfumo wa fahamu - Kuvuta Hewa chafu:
Ubongo ndio mtumiaji mkubwa wa Oxijeni tunayo ivuta. Unapovuta hewa chafu unapunguza mgawo wa Oxijeni kwenye Ubongo na hatimaye kupunguza ufanisi wake
WATANI WAFANYA MZAHA KATIKA MSIBA WA MCHEZAJI WA ZAMANI NA MMOJA WA WAANZILISHI WA TIMU YA MAJI MAJI YA SONGE
Watani wa Kiyao wakimfuatisha marehemu alivyokuwa akitembea enzi ya Uhai
wake.
Mfiwa uruusiwi kufuta huo unga ukifuta tu wanakuja na debe zima
wanakumwagia bora uwe mpole.
MZEE Abdala Alli alikuwa mmoja wa waanzilishi wa timu ya Majimaji ya Songea
wana Lizombe, yeye na wenzake watatu ndiyo walianzisha timu hiyo, Alikuwa
mzee Mbegambega, Mzee Mshamu wakiongozwa na Mhe, Laurensi Mtazama Gama hao
wote kwa sasa ni marehemu.
Mmoja wa watani wa Kabila la Wayao akimpaka unga usoni mtoto wa Kwanza wa
kiume Hamisi Abdala Alli,
Siyo Igizo ni utani kati ya Wamwela na Wayao.
Mfiwa... more »
Wednesday, December 4, 2013
TAZAMA HAPA NYIMBO 50 ZA BONGO FLAVA ZILIZOSIKILIZWA ZAIDI MTANDAONI MWAKA 2013
Zimebaki siku 26 tu hadi tuumalize mwaka 2013. Kwa kutumia akaunti maarufu za mtandao wa hulkshare zinazomilikiwa na blog tano nchini Tanzania, Bongo5 imeandaa orodha ya nyimbo zilizosikilizwa zaidi kwenye mtandao mwaka 2013. Blog hizo ni pamoja na Bongo5, Gongamx, Dj Choka, Sam Misago na Hass Baby. Pamoja na Hulkshare ndio website ya kuhifadhia nyimbo mtandaoni maarufu zaidi kuliko yote kwa sasa.
Hii ni orodha kamili ya nyimbo 50 zilizosikilizwa zaidi mtandaoni mwaka 2013.
1.Nay wa mitego ft Diamond Platnumz – Muziki Gani
14 Mar 2013
Imesikilizwa mara 93,895
Imepakuliwa mara 34,949
2.Young Killer ft Stamina & Quick Rocka – Jana na Leo
25 Apr 2013
Imesikilizwa mara 79,100
Imepakuliwa mara 31,175
3.Ben Pol – Jikubali
2 May 2013
Imesikilizwa mara 76,424
Imepakuliwa mara 30,397
4.Lady JayDEE – Yahaya
12 Jun 2013
Imesikilizwa mara 75,764
Imepakuliwa mara 12,846
5.Ney wa Mitego ft. Neyba – Salam Zao
31 Jul 2013
Imesikilizwa mara 64,062
Imepakuliwa mara 18,313
6.Diamond Platnumz- Mapenzi Basi
12 Apr 2013
Imesikilizwa mara 52,255
Imepakuliwa mara 21,589
ENDELEA KUTIZAMA NYIMBO ZAIDI KWA KUBOFYA HAPA CHINI
7.Rama Dee Ft Lady Jaydee – Kama Huwezi
3 Jul 2013
Imesikilizwa mara 52,096
Imepakuliwa mara 8,190
8.Ommy Dimpoz ft J Martins – Tupogo
1 Aug 2013
Imesikilizwa mara 47,100
Imepakuliwa mara 9,059
9.Izzo B Ft Barnaba Na Shaa – Love Me
30 Apr 2013
Imesikilizwa mara 46,151
Imepakuliwa mara 15,630
10.Chege ft Malaika- Uswazi Take Away
4 Feb 2013
Imesikilizwa mara 45,307
Imepakuliwa 23,411
11.Shetta Ft Rich Mavoko – Sina Imani
29 Mar 2013
Imesikilizwa mara 43,299
Imepakuliwa mara 16,105
12.Rich Mavoko – Roho Yangu
18 Sep 2013
Imesikilizwa mara 42,778
Imepakuliwa mara 3,330
13.Jux – Uzuri Wako
13 Mar 2013
Imesikilizwa mara 39,224
Imepakuliwa mara 14,139
14.Blue – Pesa
4 Sep 2013
Imesikilizwa mara 38,094
Imepakuliwa mara 3,908
15.Roma – 2030
4 Jan 2013
Imesikilizwa mara 37,841
Imepakuliwa mara 19,161
16.Stamina ft. Fid Q – Wazo La Leo
11 Jan 2013
Imesikilizwa mara 36,783
Imepakuliwa mara 19,127
17. Diamond Platnumz – Number 1
Imesikilizwa mara 33,707
Imepakuliwa mara 3,827
18.Cassim Mganga – I Love you
4 Jul 2013
Imesikilizwa mara 33,267
19. Quick Rocka ft. Ngwair & Shaa – My Baby
21 Jun 2013
Imesikilizwa mara 32,517
Imepakuliwa mara 10,791
20.Nikki Mbishi – Ney Wa Mitego
8 May 2013
Imesikilizwa mara 31,734
Imepakuliwa mara 11,521
21.Vanessa Mdee – Closer
Jan 2013
Imesikilizwa mara 27,838
Imepakuliwa mara 15,264
22.MwanaFA & AY Ft J Martins – Bila Kukunja Goti
26 Jun 2013
Imesikilizwa mara 27,715
Imepakuliwa mara 8,699
23.Young Killer ft Bright & Nemo – Mrs Super Star
2 Aug 2013
Imesikilizwa mara 26,664
Imepakuliwa mara 4,117
24.Lady Jaydee ft. Prof. Jay – Joto Hasira
7 Mar 2013
Imesikilizwa mara 26,316
Imepakuliwa mara 10,964
25.Linex Ft. Sunday – Kimugina
2 Aug 2013
Imesikilizwa mara 25,829
26.Nikki wa Pili ft Joh Makini – Bei ya Mkaa
30 Jul 2013
Imesikilizwa mara 24,476
Imepakuliwa mara 5,477
27.Nikki Wa Pili – Nje ya Box
15 Feb 2013
Imesikilizwa mara 20,819
Imepakuliwa mara 8,844
28.Kala Jeremiah Ft Ben Pol – Karibu Dar
13 Mar 2013
Imesikilizwa mara 20,437
Imepakuliwa mara 6,254
29.Nikki Mbishi & Godzilla Feat. Cliff Mitindo – Kill yoself
4 Feb 2013
Imesikilizwa mara 20,128
Imepakuliwa mara 12,145
30. Snura – Nimevurugwa
29 Jul 2013
Imesikilizwa mara 20,078
Imepakuliwa mara 4,780
31. Stamina ft Darasa, Warda – Mwambie Mwenzio
25 Jul 2013
Imesikilizwa mara 17,723
Imepakuliwa mara 6,244
32.Linah- Tumetoka Mbali
20 Aug 2013
Imesikilizwa mara 17,747
Imepakuliwa mara 3,438
33.Suma Mnazaleti ft Tunda – Tuko wangapi
13 Mar 2013
Imesikilizwa mara 17,630
Imepakuliwa mara 7,381
34. Madee – Sio Mimi
Imesikilizwa mara 17,411
Imepakuliwa mara 8,043
35.Ben Pol ft Alice – Waubani
8 Sep 2013
Imesikilizwa mara 17,268
Imepakuliwa mara 3552
36.Recho – Umependeza
4 Sep 2013
Imesikilizwa mara 16,894
Imepakuliwa mara 4,211
37.Lucci & Julio ft Jokate – Waters Up
2 Feb 2013
Imesikilizwa mara 16,686
Imepakuliwa mara 34,271
38.Gosby – BMS ( Baby Making Swag)
28 Jun 2013
Imesikilizwa mara 16,492
Imepakuliwa mara 3,886
39.Gosby – Monifere
9 Oct 2013
Imesikilizwa mara 16350
Imepakuliwa mara 2,626
40.Nyandu ft Young Killer, Young D & Belle 9 – Kwa Mafans
3 Jul 2013
Imesikilizwa mara 16,202
Imepakuliwa mara 6,629
41.Hard Mad – Naishi Gheto
10 Nov 2013
Imesikilizwa mara 15,573
42.Izzo B ft Ngwair and Quick Rocka – Ball Player
23 Jan 2013
Imesikilizwa 15,258
Imepakuliwa mara 8659
43.Young Dee ft Mr. Blue – Hujali
29 Jan 2013
Imesikilizwa mara 15,285
44.Suma Mnazareti Ft Richard – Umechelewa
20 Sep 2013
Imesikilizwa mara 15,052
Imepakuliwa mara 2,068
45.Mahakama ya Mapenzi – Linex.mp3
28 Jan 2013
Imesikilizwa mara 15,048
Imepakuliwa mara 9,158
46.Sajna ft. Ben Pol & Sisa Madini – Ningekuwa Single
10 Jul 2013
Imesikilizwa mara 14,463
Imepakuliwa mara 2,208
47.Bob Junior ft Vanessa Mdee – Bashasha
Imesikilizwa mara 13,792
Imepakuliwa mara 2,131
48.Chid Benz-Nakaza Roho
14 Aug 2013
Imesikilizwa mara 13,673
Imepakuliwa mara 2,439
49.Diamond – Kama Nikifa Kesho
7 Oct 2013
Imesikilizwa mara 13,542
Imepakuliwa mara 4,009
50. Cindy Rulz ft. Dunga – Let’s Wait
31 Oct 2013
Imesikilizwa mara 12,529
imepakuliwa mara 936
Bonus
51. Fid Q ft Juma Nature – Siri ya Mchezo-
19 Oct 2013
Imesikilizwa mara 10,929
Imepakuliwa mara 724
52. T.I.D Ft Kassim na Mr Blue – Tamu Asali
20 Sep 2013
Imesikilizwa mara 10,906
Imepakuliwa mara 1,866
53. Mabeste ft Peter Msechu – NISHAURI
7 Aug 2013
Imesikilizwa mara 10,692
Imepakuliwa mara 3,272
SOMA JACK WALIPER ALIVYOFUNGUKA YA MOYONI NAKUANIKA A DALASS NA KUKIRI KUWA ALI KIBA NDIO ALIYEMFUNZA MAPENZI

MOYO;
huhifadhi mengi mazito hasa ya kuumiza!
Staa mkubwa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe amejikuta
akimwaga machozi wakati akianika siri tano nzito kuhusu mapenzi katika
mahojiano (exclusive interview)
Katika ‘intavyu’ hiyo iliyofanyika
Jumatatu iliyopita kwenye Ofisi za Global Publishers, Bamaga-Mwenge
jijini Dar kuanzia saa 8:44 alasiri hadi saa 10:44 jioni, Wolper
alifunguka vitu vingi.
KISA/MKASA
Akizungumza kwa masikitiko, uchungu na majuto, Wolper alisema hawezi kumsahau mwanaume huyo ambaye ni Abdallah Mtoro ‘Dallas’ kwa namna alivyomwingia kijanja na kutaka kumvunjia heshima aliyoijenga karibia miaka kumi nyuma.
Akizungumza kwa masikitiko, uchungu na majuto, Wolper alisema hawezi kumsahau mwanaume huyo ambaye ni Abdallah Mtoro ‘Dallas’ kwa namna alivyomwingia kijanja na kutaka kumvunjia heshima aliyoijenga karibia miaka kumi nyuma.
ALIANZIA WAPI NA DALLAS?
“Siku ya kwanza Dallas alinipigia simu na kuniambia aliniona Magomeni (Dar). Naikumbuka sana siku hiyo, ilikuwa baada ya mizunguko yangu, mwanzoni sikupokea simu yake kwa sababu ilikuwa namba ngeni kwangu.
“Nilimsikiliza sana. Jamani yule mwanaume anaongea kwa ushawishi wa hali ya juu mno. Nilishangaa aliponieleza kila kitu kuhusu familia yangu na nyumbani kwetu. Kumbe tayari alishaunda urafiki na baba yangu (mzee Massawe).
“Siku ya kwanza Dallas alinipigia simu na kuniambia aliniona Magomeni (Dar). Naikumbuka sana siku hiyo, ilikuwa baada ya mizunguko yangu, mwanzoni sikupokea simu yake kwa sababu ilikuwa namba ngeni kwangu.
“Nilimsikiliza sana. Jamani yule mwanaume anaongea kwa ushawishi wa hali ya juu mno. Nilishangaa aliponieleza kila kitu kuhusu familia yangu na nyumbani kwetu. Kumbe tayari alishaunda urafiki na baba yangu (mzee Massawe).
“Mwanzoni nilidhani ni tapeli.
Nikamkatia simu. Akaendelea kunipigia na nilipoona imekuwa kero kubwa
nilipokea. Ili kuthibitisha anawajua wazazi wangu, alinitajia namba zao
za simu ambazo ni za kweli.
“Pamoja na hilo nilimfanyia nyodo, si unajua mtoto wa kike? Lakini aliniongelesha kwa upole hadi nikapunguza nyodo zangu.
“Pamoja na hilo nilimfanyia nyodo, si unajua mtoto wa kike? Lakini aliniongelesha kwa upole hadi nikapunguza nyodo zangu.
“Aliniuliza nataka anifungulie biashara
gani. Nikamwambia biashara ya nguo. Akaniuliza nataka mtaji kiasi gani.
nikamwambia dola laki moja kwa sababu nilikuwa sitaki fremu moja,
nilitaka nyumba nzima. Akaniambia hakuna tatizo.
“Pia aliniuliza naishi wapi? Nikamwambia Sinza (Dar) alionesha dharau kwenye simu akaniambia atanihamishia Mbezi Beach.
“Pia aliniuliza naishi wapi? Nikamwambia Sinza (Dar) alionesha dharau kwenye simu akaniambia atanihamishia Mbezi Beach.
“Aliniuliza natembelea gari gani?
Nikamwambia Toyota Noah. Akaniambia ningependa aninunulie gari gani?
Nikamjibu Toyota Discovery lakini yeye akasema ataninunulia Toyota
Harrier.
“Kweli baada ya siku mbili-tatu
nililetewa Toyota Harrier nyeusi nyumbani. Niliogopa isijekuwa mtego
nikaingia kwenye matatizo hivyo nilimzungusha mtu aliyeniletea hadi
Sinza-Mori nikamwambia apaki kwenye kituo cha teksi, nikaenda na dereva
nikalichukua hadharani ili lolote likitokea nipate msaada.
“Nilikabidhiwa funguo za lile gari na
documents zake, nikaondoka nalo hadi nyumbani kwangu. Kesho yake Dallas
alimtuma mtu aniletee dola za Kimarekani 15,000 (zaidi ya Sh. milioni
24). Nilipouliza za nini aliniambia ni kwa ajili ya shopping ya
kutembelea Harrier niachane na zile swaga za kwenye Noah (fedha
inaongea). Kisha akanitumia cheni ya dhahabu.
“Siku iliyofuata alinitumia Sh. milioni
15 nipeleke nyumbani nikawaambie wazazi nimepata mchumba ambaye
angeenda kujitambulisha baadaye. Niliwaambia ni Dallas ambaye walikiri
kumfahamu kwa sababu alishawapigia simu na kujitambulisha kuwa ni mkwe
wao.”
AMESHAKUTANA NA DALLAS?
“Hadi hapo nilikuwa sijamuona Dallas kwa sura na fedha nilikuwa natumiwa kila siku.
“Wakati hayo yakiendelea akaagiza nihamishiwe Mbezi Beach na kununuliwa lile gari lililoibua mzozo BMW X6.
“Nakumbuka siku niliyokabidhiwa lile gari nililia sana. Sikuamini macho yangu kwa sababu Dallas aliniambia amenitumia kazawadi kumbe ni BMW X6 (lina stori ndefu inakuja)!
“Hadi hapo nilikuwa sijamuona Dallas kwa sura na fedha nilikuwa natumiwa kila siku.
“Wakati hayo yakiendelea akaagiza nihamishiwe Mbezi Beach na kununuliwa lile gari lililoibua mzozo BMW X6.
“Nakumbuka siku niliyokabidhiwa lile gari nililia sana. Sikuamini macho yangu kwa sababu Dallas aliniambia amenitumia kazawadi kumbe ni BMW X6 (lina stori ndefu inakuja)!
“Kumbuka mwanzoni nilikuwa na boyfriend
ambaye tulipendana sana lakini hatukupanga kufunga ndoa. Nilimweleza
kila kitu akakubaliana na mimi japokuwa aliumia.
“Maskini! Kuanzia hapo nikawa nimeachana na yule boyfriend wangu lakini hakukuwa na namna kwa sababu niliamini nimepata mchumba wa kunioa.
“Maskini! Kuanzia hapo nikawa nimeachana na yule boyfriend wangu lakini hakukuwa na namna kwa sababu niliamini nimepata mchumba wa kunioa.
ATAKIWA KUBADILI DINI
“Baadaye Dallas aliniambia nimeshakuwa mchumba wake hivyo nibadili dini. Kweli nilibadili nikawa Muislam na jina langu likawa Ilham. Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana maishani mwangu kwa sababu nilionekana ni muasi katika dini yangu ambayo mama ni mzee wa usharika na mwimba kwaya, baba ni mtu wa kanisani sana.”
“Baadaye Dallas aliniambia nimeshakuwa mchumba wake hivyo nibadili dini. Kweli nilibadili nikawa Muislam na jina langu likawa Ilham. Hicho kilikuwa kipindi kigumu sana maishani mwangu kwa sababu nilionekana ni muasi katika dini yangu ambayo mama ni mzee wa usharika na mwimba kwaya, baba ni mtu wa kanisani sana.”
NINI KILIFUATA?
“Siku moja nilikuwa Tanga nashuti filamu, nilikuwa nikitoka hapo niende Morogoro. Dallas alinipigia simu akaniambia yupo Nairobi (Kenya) anakuja Tanzania. Nilimwambia nipo Tanga akaniambia atanifuata kule. “Niliendelea kupiga mzigo. Zilipita saa nyingi, baadaye nikiwa na kruu yangu, Dallas alinipigia simu akaniambia ameniona.
“Nilikataa, akaniambia namna nilivyo, nguo nilizovaa na watu niliokuwa nao, alipatia. Kumbe alikuja na Toyota Prado.
“Siku moja nilikuwa Tanga nashuti filamu, nilikuwa nikitoka hapo niende Morogoro. Dallas alinipigia simu akaniambia yupo Nairobi (Kenya) anakuja Tanzania. Nilimwambia nipo Tanga akaniambia atanifuata kule. “Niliendelea kupiga mzigo. Zilipita saa nyingi, baadaye nikiwa na kruu yangu, Dallas alinipigia simu akaniambia ameniona.
“Nilikataa, akaniambia namna nilivyo, nguo nilizovaa na watu niliokuwa nao, alipatia. Kumbe alikuja na Toyota Prado.
WOLPER MORO, DALLAS DAR
“Tulipomaliza kurekodi Tanga tulikwenda Morogoro, yeye aliniambia anaelekea Dar. Tulikuwa tunawasiliana. Nilipomaliza kurekodi Moro nilirejea Dar. Hapo ndipo vituko vikawa juu ya vituko.
“Tulipomaliza kurekodi Tanga tulikwenda Morogoro, yeye aliniambia anaelekea Dar. Tulikuwa tunawasiliana. Nilipomaliza kurekodi Moro nilirejea Dar. Hapo ndipo vituko vikawa juu ya vituko.
“Niliambiwa mara kaonekana sehemu akiwa
na mwanamke au wanawake. Mimi sikujali kwa sababu nilipomuuliza
aliniambia hatuwezi kuonana kwa sababu kipindi hicho alikuwa katika
swaumu hivyo akionana na mimi nitamharibia. (ulikuwa mwezi mtukufu).
BADO HAWAJAKUTANA?
“(Mguno) Hapo bado hatujakutana lakini yupo mjini na amejaa tele kwenye kumbi za starehe.
“Baada ya kumaliza swaumu, siku moja aliniambia anakuja nyumbani Mbezi Beach. Niliwaalika marafiki zangu tukapika vyakula, tukafanya usafi na kufukiza udi chumbani. Nilitandika mashuka meupe kitandani na kujipara kisha nikavaa ushungi kuanzia mchana nikakaa kama malkia nikimsubiri mchumba.
“(Mguno) Hapo bado hatujakutana lakini yupo mjini na amejaa tele kwenye kumbi za starehe.
“Baada ya kumaliza swaumu, siku moja aliniambia anakuja nyumbani Mbezi Beach. Niliwaalika marafiki zangu tukapika vyakula, tukafanya usafi na kufukiza udi chumbani. Nilitandika mashuka meupe kitandani na kujipara kisha nikavaa ushungi kuanzia mchana nikakaa kama malkia nikimsubiri mchumba.
“Huwezi amini, hadi giza linaingia
Dallas hakutia mguu. Nilipataje aibu kwa rafiki zangu waliotaka kumuona
huyo mchumba? Ninyi acheni tu!
“Nilipomuuliza aliniambia alipata dharura kuna biashara alikuwa anafanya
“Nilipomuuliza aliniambia alipata dharura kuna biashara alikuwa anafanya
HATIMAYE WAKUTANA LAKINI…
“Nilikasirika sana, nikasema huyu ni mchumba gani asiyetaka kuja kwangu? Nikampa muda wa siku tatu aje nyumbani na alete nguo zake zote. Kweli, siku ya tatu, asubuhi nilimsikia mtu akiita ‘Ilham Wolper Dallas’. Nilishajua sauti yake kupitia simu hivyo nilimkaribisha na nguo zake nikaingiza ndani. Lakini cha kushangaza alikuja na pikipiki!
“Nilikasirika sana, nikasema huyu ni mchumba gani asiyetaka kuja kwangu? Nikampa muda wa siku tatu aje nyumbani na alete nguo zake zote. Kweli, siku ya tatu, asubuhi nilimsikia mtu akiita ‘Ilham Wolper Dallas’. Nilishajua sauti yake kupitia simu hivyo nilimkaribisha na nguo zake nikaingiza ndani. Lakini cha kushangaza alikuja na pikipiki!
“Alishinda nyumbani siku hiyo maana
kuna ndugu zake walikuja. Hatukufanya chochote. Dallas aliishia kunibusu
shavuni kisha jioni akaondoka.
“Mjini kukawa hakukaliki. Natumiwa picha akiwa na wanawake tofautitofauti. Mmoja wa wanawake hao niliambiwa eti ana ‘ngoma’! Jamani hii dunia ina kichaa!
“Mjini kukawa hakukaliki. Natumiwa picha akiwa na wanawake tofautitofauti. Mmoja wa wanawake hao niliambiwa eti ana ‘ngoma’! Jamani hii dunia ina kichaa!
“Muda ukasonga, vitimbi vikawa vingi.
Dallas simuoni. Muda wa kukaa kwenye ile nyumba uliisha hivyo nikahama
na nikamwambia akachukue nguo zake.
UCHUMBA WAVUNJIKA, SASA ANAPUMZIKA HAPA
“Baadaye uchumba ukavunjika tena mimi ndiyo nilimwambia simtaki tena. Nilikaa muda hadi baadaye nilipopata mwanaume wangu wa sasa. Anani-control vizuri kwa sababu kanipita umri na ana busara. Tunapendana sana. Najuta kumfahamu Dallas. Siwezi kusahau tukio hilo katika maisha yangu. Dallas alicheza na hisia za moyo wangu. (akaangua kilio) Niliteseka sana. Ni Mungu tu anajua…
“Baadaye uchumba ukavunjika tena mimi ndiyo nilimwambia simtaki tena. Nilikaa muda hadi baadaye nilipopata mwanaume wangu wa sasa. Anani-control vizuri kwa sababu kanipita umri na ana busara. Tunapendana sana. Najuta kumfahamu Dallas. Siwezi kusahau tukio hilo katika maisha yangu. Dallas alicheza na hisia za moyo wangu. (akaangua kilio) Niliteseka sana. Ni Mungu tu anajua…
VIPI KURUDIA UKRISTO?
“Nimekaa muda siendi kanisani. Nilikuwa najifungia ndani nalia kama mama yangu alivyokuwa anafanya. Siku moja nilimwambia mwanaume wangu akaniambia kuliko kulia kila siku bora nirudi kanisani. Ndipo nikarudia ukristo. Kwa sasa nasali Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama, Dar,” alisema.
“Nimekaa muda siendi kanisani. Nilikuwa najifungia ndani nalia kama mama yangu alivyokuwa anafanya. Siku moja nilimwambia mwanaume wangu akaniambia kuliko kulia kila siku bora nirudi kanisani. Ndipo nikarudia ukristo. Kwa sasa nasali Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama, Dar,” alisema.
MBALI NA DALLAS
Kwa mara ya kwanza Wolper alikubali kuorodhesha listi ya wanaume aliowahi kuwa nao kimapenzi kwa kuwachambua mmoja mmoja.
Kwa mara ya kwanza Wolper alikubali kuorodhesha listi ya wanaume aliowahi kuwa nao kimapenzi kwa kuwachambua mmoja mmoja.
ALI KIBA
Bila kupepesa macho, Wolper alikiri kuwa msanii wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ndiye aliyemfundisha mapenzi: “Ni kitambo kidogo. Wote hatukuwa mastaa lakini yeye alifanikiwa kuchomoka. Kabla ya Ali (Kiba) nilikuwa na mwanaume lakini hatukuduu kwa maana ya utu uzima, ilikuwa yale ya kitoto. Lakini Ali ndiye hasa aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi.
Bila kupepesa macho, Wolper alikiri kuwa msanii wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ndiye aliyemfundisha mapenzi: “Ni kitambo kidogo. Wote hatukuwa mastaa lakini yeye alifanikiwa kuchomoka. Kabla ya Ali (Kiba) nilikuwa na mwanaume lakini hatukuduu kwa maana ya utu uzima, ilikuwa yale ya kitoto. Lakini Ali ndiye hasa aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi.
KWA NINI WALIACHANA?
“Ali akawa staa. Alipokwenda nje nikasikia wanawake wanamshobokea. Sasa mimi sikutaka karaha nikakaa pembeni lakini jamaa ni mtu poa sana na tukikutana tunasalimiana freshi kabisa.”
“Ali akawa staa. Alipokwenda nje nikasikia wanawake wanamshobokea. Sasa mimi sikutaka karaha nikakaa pembeni lakini jamaa ni mtu poa sana na tukikutana tunasalimiana freshi kabisa.”
DIAMOND VIPI?
“Ni kweli niliwahi kuwa na Diamond (msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul). Tulikuwa na uhusiano lakini pia alikuwa mshirika wa kibiashara (hataki kuitaja). Yeye alikuwa hawezi kulala bila kuniona, lakini tulikaa kama mwezi mmoja, kwa sasa amebaki kuwa rafiki yangu na siyo mpenzi tena kama zamani,” alisema Wolper.
“Ni kweli niliwahi kuwa na Diamond (msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul). Tulikuwa na uhusiano lakini pia alikuwa mshirika wa kibiashara (hataki kuitaja). Yeye alikuwa hawezi kulala bila kuniona, lakini tulikaa kama mwezi mmoja, kwa sasa amebaki kuwa rafiki yangu na siyo mpenzi tena kama zamani,” alisema Wolper.
VIPI KUHUSU JUX?
“Jux (msanii wa Bongo Fleva, Juma Khalid) nilikuwa naye kabla ya Dallas na yule mwanaume wangu niliyeachana naye wakati wa Dallas. Katika maisha yangu nilimpenda sana Jux. Siyo marioo ni mwanaume mtafutaji aliyejiamini. Kwa sasa sipo naye. Dallas pia alichangia mimi kuachana na Jux,” alimalizia Wolper ambaye kwa sasa ana mwanaume asiyependa kumwanika.
“Jux (msanii wa Bongo Fleva, Juma Khalid) nilikuwa naye kabla ya Dallas na yule mwanaume wangu niliyeachana naye wakati wa Dallas. Katika maisha yangu nilimpenda sana Jux. Siyo marioo ni mwanaume mtafutaji aliyejiamini. Kwa sasa sipo naye. Dallas pia alichangia mimi kuachana na Jux,” alimalizia Wolper ambaye kwa sasa ana mwanaume asiyependa kumwanika.
Friday, November 29, 2013
BERKO KULIPWA MSHAHARA MKUBWA KULIKO KASEJA
Kipa wa zamani wa Yanga, Yaw Berko
anatua nchini leo akitokea kwao Ghana akiwa kipa ghali zaidi kwa kuwa atalipwa
mshahara mkubwa hata kuliko Juma Kaseja wa Yanga.
Berko anatua nchini saa nne asubuhi
kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) na mara moja
atakwenda kumalizia mazungumzo na Simba na tayari wamekubaliana mshahara wake
utakuwa dola 1,500 (Sh 2,400,000), kwa mwezi.
Mabingwa Yanga wanamlipa Kaseja
aliyekuwa ameachwa na Simba Sh milioni 2, sawa na mshambuliaji mwingine wa
Yanga, Mrisho Ngassa ambaye pia aliichezea Simba msimu uliopita.
Lakini katika mazungumzo yake, kipa
huyo ameutaka uongozi wa Simba kumhakikishia kwamba kipa Abel Dhaira raia wa
Uganda anabeba virago vyake na kuondoka.
“Berko amesema yuko tayari kuja nchini
na kuanza kazi lakini asingependa hata kidogo kuona Dhaira yupo. Ndiyo kilikuwa
kitu cha kwanza ambacho hakihitaji kukiona na kweli tumefanya hivyo kwa kuwa
hata Dhaira mwenyewe ameonyesha anataka kuondoka,” kilieleza chanzo kutoka
ndani ya Simba.
Hata hivyo, Simba italazimika
kumsajili kwa nusu msimu tu kwa kuwa TFF tayari imetangaza kuanzia msimu ujao,
imepitisha sheria ya timu kutosajili makipa wa kigeni.
Berko aliondoka nchini Yanga ikiwa
inamhitaji, lakini ililazimika kumtumia Ally Mustapha ‘Barthez’ aliyekuwa kipa
wa pili baada ya kipa huyo kuonyesha usumbufu na maringo huku viongozi
wakilalamika alikuwa si mtu anayejituma.
Saturday, October 5, 2013
MMEONA MUZIKI WA MSANII SHILOLE UNAVYOCHEZWA JUKWAANI ?, ADAIWA KUNYONYWA MATITI MBELE YA UMATI WA MASHABIKI WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA.
Shabiki huyu sijui alimruhusu amnyonya maziwa Shilole baada ya kumuita jukwaani ili wach
eze wote. Mhhhhh hatari kweli kweli.
Kazi ipo !!!, Shilole akionyesha kulegea baada ya kunyonywa na shabiki wake huyu mwanaume.
jamaa akifaiti ziwa la Shilole
Angalau hapa pamekaa vyema kwa uchezaji japo kidogo !!!.
Aina hii ndiyo inaanza hivi.
Hii nayo ni aina nyingine pindi anapokuwa anacheza na shabiki, haki ya nani balaa tupu.
Huyu ndo Shilole katikati ya mwili wa mwanaume ambaye anadaiwa kuwa ni
shabiki wake, hii ni aina nyingine ya uchezaji wa muziki wa Shilole
namna unavyochezwa.
Sijui huu ndiyo muziki gani unaochezwa hivi, sidhani kama mtu atasutwa kufanishwa na kitendo hiki kinachofanywa na watu wenye jinsia mbili tofauti katika faragha.
Saturday, September 21, 2013
MASOGANGE NA MDOGO WAKE WAACHIWA HURU
Tegemea picha zaidi za ‘asset’ ya Agnes Gerald aka Masogange kwenye Instagram sababu video vixen huyo ni mtu huru kabisa.
Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi la
leo, Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg, nchini Afrika Kusini
imemwachia huru mrembo huyo baada ya kulipa faini ya R30,000 ambazo ni
sawa na shilingi milioni 4.8 za Tanzania, kubeba kemikali zinazotumika
kutengeneza dawa za kulevya.
Naye Melissa Edward ameachiwa huru na mahakama hiyo, baada ya kukosekana ushahidi wowote wa kumtia hatiani.
Habari hiyo kwenye gazeti la Mwananchi inaeleza kwa urefu:
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa
Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini(Hawk), Kapteni Paul Ramaloko alisema
Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa
za kulevya, bali kemikali aina ya ephedrine.
Mahakama hiyo ilibaini kuwa, Melissa
hana hatia kwa kuwa ilionekana kuwa amemsindikiza Masogange, ambaye
alimwomba amsaidie kubeba mzigo huo.
“Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa
tu kumsaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini hayakuwa yake. Mizigo yote
iliandikwa jina la Agness Gerald na si Melissa,” gazeti la Mwananchi
limemnukuu Kapteni Ramaloko.
Alisema, Melissa alijitetea kuwa hakuwa
amesafiri pamoja na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na
Masogange alimwomba amsaidie kubeba mizigo hiyo, kwani ilikuwa mikubwa.
Kwa sheria za Afrika Kusini kubeba
kemikali zozote ambazo zimepigwa marufuku ni kosa la jinai kisheria,
hivyo mahakama iliamuru Masogange ahukumiwe kwenda jela kwa miezi 30
(miaka miwili na miezi mitano) au alipe faini ya R30, 000 (sawa na Sh4.8
milioni).
Hata hivyo, Kapteni Ramaloko alisema mdhamini wa Masogange alilipa nusu ya fedha na kwamba zinazobaki amalizie baadaye.
Alisema kutokana na kutomalizia kulipa
fedha hizo ataendelea kubaki nchini humo hadi atakapomaliza kulipa nusu
ya faini iliyobaki.
Masogange na mwenzake walipokamatwa na SARS ilielezwa walikuwa wamebeba dawa za kulevya aina ya
Methamphetamine, lakini Mahakama juzi ilithibitisha walikamatwa na kemikali aina ya Ephedrine, ambayo siyo dawa za kulevya.
Wakati Kamishna Mkuu wa Kitengo cha
Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini, Geofrey Nzowa alipoulizwa na Mwananchi
Jumamosi juzi alisema mzigo walioubeba Masogange na mwenzake haukuwa ni
dawa za kulevya bali ni kemikali za dawa za kulevya, lakini Msemaji wa
Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini, (SARS), Marika Muller alieleza kuwa
timu ya SARS ina uhakika kuwa mabegi sita yaliyokamatwa Julai 5 ni dawa
za kulevya aina ya Methamphetamine.
Jana, Muller alipoambiwa kuwa Watanzania
hao wameachiwa huru baada ya kulipa faini na mmoja kuachiwa huru kwa
kuwa Mahakama imeridhika kuwa hazikuwa methamphetamine bali kemikali
aina ya Ephedrine, alirudia tena na kueleza kuwa, mamlaka hiyo ina
uhakika na kazi yake na iwapo mahakama imewaachia huru basi yeye hana la
kusema zaidi.
“Kazi yetu kubwa ni kukamata mizigo
haramu inayopitishwa uwanja wa ndege, kama Mahakama imeona kuwa si dawa
za kulevya, hatuna la kuongeza. Kikubwa tumemaliza kazi yetu,” alisema
Muller kwa kujiamini.
Hata hivyo, Nzowa jana akizungumzia
kuachiwa huru kwa Watanzania hao, alionyesha kushangazwa jinsi Mahakama
ilivyotoa adhabu ndogo.
“Hii ni ajabu sana. Kama watu wamebeba
mzigo wenye thamani ya Sh6.8 bilioni wanapigwa faini ya milioni nne,
hawataogopa kufanya hiyo biashara. Hao watu ni hatari sana,” alisema
Nzowa.
Alipoulizwa iwapo wakirudi Tanzania
wanaweza kushtakiwa, Nzowa alisema kitengo chake hakitaweza kuwashtaki
tena kwa sababu wanaweza kujitetea kuwa tayari walishahukumiwa,
isipokuwa Mwendesha Mashtaka aliyekuwa akisimamia kesi yao anaweza
kukata rufaa.
“Iwapo Mwendesha Mashtaka wa huko
akikata rufaa kwa kuona adhabu aliyopewa mhalifu huyo ni ndogo, anaweza
kufanya hivyo,” alisema Nzowa.
Nzowa alisema, inasikitisha kuwa wakati mapambano ya biashara hiyo yakiwa yanaendelea Tanzania, watuhumiwa hao wanaachiwa.
“Adhabu waliyopewa ni ndogo hasa wakati
huu ambao Tanzania tunachafuka kwa tuhuma hizi. Lazima kitu kifanyike
kubadili hali halisi hapa nchini,” alisema.
Nzowa alieleza kuwa alikwenda Afrika
Kusini tangu Septemba Mosi kuwahoji wasichana hao ambao hata hivyo
hawakuweza kusema lolote la kuisaidia polisi.
Masogange aliandika kwa maandishi kuwa
ni kweli mzigo ulikuwa wa kwake, lakini akasema mdogo wake, ambaye ni
Melissa, hajui lolote na alikuwa amemsaidia.
Julai 5, mwaka huu Masogange na Melissa
walikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo
wakidaiwa wamebeba kilo 150 zilizodaiwa kuwa ni dawa za kulevya aina ya
Methamphetamine zenye thamani ya Sh6.8 bilioni.
Dawa hizo zilizokuwa zimepakiwa katika
mabegi makubwa sita, zinatajwa kuwa ni kiwango kikubwa kukamatwa katika
historia ya SARS ndani ya uwanja huo unaotumiwa na mataifa makubwa
duniani.
Taarifa za kukamatwa kwa wasichana hao
zilipamba kurasa mbalimbali za magazeti ndani na nje ya Tanzania, jambo
lililosababisha Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe kuchukua hatua
za kuusafisha Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere.
Baada ya uchunguzi wa Dk Mwakyembe ambao
ulibaini kuwapo mchezo mzima uliochezwa wakati Masogange na Melissa
walipokuwa uwanja wa ndege.
Agosti 17 alitoa agizo la kufukuzwa
kazi, Koplo Juliana Thadei, Jackson Manyoni, Yusuph Daniel Issa, Koplo
Ernest na Mohamed Kalugwan.
Mwakyembe alisema katika hali isiyokuwa
ya kawaida mfanyabiashara ambaye hakuwa na tiketi ya kusafiri siku hiyo,
baadaye alibadili mawazo hapohapo na kuamua kuondoka siku hiyo kwenda
Afrika Kusini na kulipia faini ya dola 60 (Sh96, 000) ili kupata tiketi.
Pia Mwakyembe aliliagiza Jeshi la Polisi
kushirikiana na Polisi wa Kimataifa (Interpol) kumkamata mfanyabiashara
anayedaiwa kumsaidia Masogange kusafirisha dawa za kulevya ambaye
alitoweka na mabegi matatu ya dawa hizo huko Afrika Kusini.
Source: Mwananchi
Daktari FEKI akamatwa katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar
DAKTARI anayedaiwa kuwa bandia amekamatwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, akiwa na vitambulisho bandia vya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS) akisomea Shahada ya Pili.
‘Daktari’ huyo ambaye amekuwa akitafutwa na uongozi wa
chuo kwa zaidi ya mwaka alikamatwa jana asubuhi akiwa hospitalini hapo karibu na
jengo kilimo kitengo cha meno.
Katika kitambulisho chake cha kupigia kura
anatambulishwa kwa jina la Dismas John Macha aliyezaliwa mwaka 1979 Kilimanjaro
na anaishi maeneo ya Upanga Magharibi, Dar es Salaam.
Gazeti hili, lilimshuhudia mtuhumiwa huyo akiwa katika
kituo cha usalama cha Muhas na kupekuliwa na askari Polisi wa Muhimbili, Anthony
Mwamatepela na kukutwa akiwa na vifaa vya udaktari .
Baadhi ya vifaa alivyokutwa navyo ni pamoja na koti
jeupe la udaktari na stetoskopu ambacho ni kifaa cha kusikilizia mapafu
yanavyofanya kazi na mapigo ya moyo.
Pia alikuwa na begi jeusi lenye aina mbalimbali za
dawa, vitambulisho na karatasi nyingi, lakini alipoulizwa alidai kuwa hizo ni
dawa zake.
Macha alikutwa pia na vitambulisho vitatu tofauti,
kimoja kikimtambulisha kuwa mwanafunzi wa Muhas wa Shahada ya Pili ya Udaktari
(Masters of Medicine ) yenye jina la Macha Dismas kikionesha kusajiliwa kwa
namba 60520/2011 na kumaliza muda wake Septemba 30 mwakani. Kitambulisho kingine
kilimtambulisha kwa jina la Macha Rogers anayesoma Shahada hiyo hiyo ikionesha
kuwa anamaliza masomo yake mwakani.
Alikutwa pia na kitambulisho kinachomwonesha kuwa
mwanafunzi wa Shahada ya Kwanza na kadi ya anuani yenye jina la Amos Nnko ambaye
ni Ofisa Rasilimaliwatu wa Chuo hicho.
Akizungumzia alivyomkamata askari wa chuo hicho,
Fulgence Semfukwe alisema walimkamata baada ya kupata taarifa za yeye kuwa
maeneo hayo na kupanga mbinu za kumkamata.
Alisema saa 4.45 asubuhi jana alimkuta kwenye jengo la
meno na kumwomba kwa nafasi yake ya udaktari amsaidie tatizo lake na hivyo
waongee pembeni, naye bila wasiwasi akakubali. Alimwuliza anatibu magonjwa gani
naye kumjibu anatibu maradhi ya aina nyingi na kumwomba kitambulisho na yeye
kumpa cha kwake.
Baada ya hapo alishituka na kudai kuwa ni daktari wa
Mwananyamala na amekuja hapo kwa ajili ya kuona wagonjwa wake wa dharura ndipo
alipokamatwa na kupelekwa kituo cha Polisi.
Alisema amekuwa akiwachenga kwa muda mrefu kutokana na
kuwa kila walipopewa taarifa yuko wodi au sehemu Fulani hawakumkuta kwani
walipishana naye baada ya kuvua koti na kuweka kwenye begi lake
jeusi.
Akizungumza na gazeti hili, Macha limweleza mwandishi
wa habari hizi kuwa yeye ni mwanafunzi ambaye anaelewa masuala yote ya matibabu,
lakini alifeli chuoni hapo mwaka jana.
Alidai kuwa dawa alizokutwa nazo ni zake kwani ana
matatizo katika njia ya mkojo na kifua huku akiamua kufanya hivyo kutokana na
ugumu wa maisha.
“Uwezo wa kutibu ninao na nimesoma katika chuo hiki,
lakini mwaka jana nilifeli ndiyo maana nikaamua kuwa hivi,”
alisema.
Ofisa Uhusiano wa Muhas, Hellen Mtui alisema kutokana
na kukamatwa na nyaraka akijitambulisha kuwa mwanafunzi wa ‘Masters of
Medicine’, ambaye anaweza kutibu watu hawana uhakika na idadi ya watu ambao
ameshatapeli hospitalini hapo.
Kuhusu kusoma Muhimbili, Mtui alikana akisema baada ya
kupekua nyaraka za chuo hawakubaini jina la mwanafunzi wa aina hiyo na katika
vyeti vyake bandia vinaonesha kusainiwa na Mkuu wa Chuo aliyekuwapo kabla chuo
hakijapanda hadhi na kuwa chuo kikuu.
Mtui alisema baada ya kumkamata na kumpiga picha akiwa
na mavazi ya udaktari, kumpekua na kumhoji walimpeleka katika kituo cha Polisi
cha Selander Bridge kwa mahojiano na uchunguzi zaidi.
Subscribe to:
Posts (Atom)















