Wednesday, December 26, 2012

HAYA NDIO MAGAZETI YA DEC 24 2012, UDAKU MICHEZO NA HARDNEWS


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Mandela kusalia hospitalini Krismasi

Nelson Mandela
Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Nelson Mandela atasalia hospitalini msimu huu wa Krismasi.
Bwana Mandela ambaye ni rais mweusi wa kwanza nchini Afrika Kusini, alilazwa hospitali wiki mbili zilizopita kufuatia maambukizi ya mapafu na uvimbe au mawe kwenye kibofu.
Kuna wasi wasi mkubwa nchini Afrika kuhusu afya yab rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 94.
Mandela alifungwa miaka 27 baada ya kupatikana na hatia ya kuongoza uasi dhidi ya serikali ya Wazungu walio wachache nchini humo.
Raia wengi wa nchi hiyo wanamuona kama baba wa taifa kutokana na juhudi zake ya kupigania uhuru wa taifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na serikali, Bwana Mandela atasherehekea siku kuu ya Krismasi akiwa hospitalini.
Mwandishi wa BBC, mjini Johannesburg, anasema kila kukicha kuna hali ya wasi wasi kuhusu afya ya rais huyo wa zamani.
Awali kulikuwa na matumaini kuwa Bwana Mandela huenda akaruhusiwa kwenda nyumbani, lakini madaktari wake wanasema hawako tayari kumruhusu Bwana Mandela kwenda nyumbani.
Licha ya rais Zuma kutangaza kuwa Afya ya rais huyo wa zamani sio nzuri sana, Rais Zuma amesema anaendelea kupata nafuu.
Serikali ya Afrika Kusini imesema Mandela anatibiwa kufuatia maambukizi ya Mapafu katika hospitali moja mjini Pretoria.

Watu watano wauawa Nigeria

Watu wakisimama mbele ya Kanisa
Picha ya watu waliosimama mbele ya Kanisa Katoliki lililoshambuliwa nchini Nigeria, Desemba 25,2011
Majeshi ya usalama kaskazini mwa Nigeria wamesema watu wenye silaha wamekishambulia kijiji kimoja chenye wakaazi wengi Wakristo na kuua watu watano na wengine wanne kujeruhiwa.
Msemaji wa jeshi ameiambia BBC kuwa washambuliaji waliwafyatulia risasi waumini wakiwa Kanisani katika ibada ya mkesha wa Krismasi.
Amesema mtuhumiwa mmoja wa mashambulio hayo amekamatwa, na ulinzi katika eneo hilo umeimarishwa ili kuwahakikishia usalama wakaazi wa eneo hilo.
Msemaji huyo amesema nyumba kadha karibu na kanisa lililoshambuliwa zilitiwa moto.
Hakuna kikundi kilichodai kuhusika na mashambulio hayo katika jimbo la Yobe, lakini katika siku za nyuma kikundi cha Kiislam cha Boko Haram kiliwashambulia Wakristo katika jimbo hilo.

Wakristu waadhimisha siku ya Krismasi

 
Papa Mtakatifu Benedict
Papa Mtakatifu Benedict akiongoza misa ya Krismasi
Wakristo kote duniani hii leo wanaadhimisha siku kuu ya Krismasi, siku ambayo wanakumbuka kuzaliwa kwa Yesu Kristu mjini Bethlehem.
Mjini Bethlehem kwenyewe, wakaazi wa mji huo waliadhimisha siku hiyo katika kanisa na Nativity lililojengwa miaka elfu moja mia saba iliyopita, eneo ambalo linaaminika ndiko Yesu alikozaliwa.
Mjini Vatican, Papa Mtakatifu Benedict XVI, aliongoza ibada ya Krismasi katika kanisa la St Peter's Basilica.
Akiongea wakati wa Ibada hiyo papa alitoa wito kwa Wakristo kumrejela Mungu.
Aliwaombia raia wa Israel na Palestina ili waweze kuishi kwa amani.
Raia wakiadhimisha Krismasi
Raia wa Viena wakiadhimisha Krismasi
Vile vile papa Benedict aliwaombea raia wa Lebanon, Syria na Iraq.
Misa hiyo ambao kila mwaka huadhimisha saa sita za usiku iliadhimisha saa mbili mapema ili kumruhusu papa Benedict mwenye umri wa miaka 85 kumpunzika.
Baadaye hii leo,papa Benedikto atatoa ujumbe wake na baraka, unaojulikana kama Urbi et Orbi, kwa mji wa Roma na kwa Ulimwengu, kutoka kwa roshani ya St Peter's mjini Roma.
Mjini Bethlehem, kiongozi wa kanisa la katoliki pia aliwaomba raia wa Palestina na kusema wazi kuwa anaunga mkono kubuniwa kwa taifa huru la Wapalestina.
Fouad Twal alisema Krismasi hii itakuwa sherehe ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu na pia kuzaliwa kwa taufa jipya la Palestina.
Wakristu wakiadhimisha Krismasi
Wakristu wakiadhimisha Krismasi
Hata hivyo alionya kuwa harakati za kaufikiwa kwa taifa huru la Palestina bado hazijamalizika na itahitaji ushirikiana zaidi.
Askofu huyo ambaye alizaliwa nchini Jordan aliongoza maandamana kutoka mji wa kale wa Jerusalem hadi ukingo wa Magharibi mwa mto Jordan, kupitia vizuizi vinavyogawanya mataifa ya Palestina an Israel na kituo cha ukaguzi kilichojengwa na serikali ya Israel.
Barani Afrika Wakirstu wa madhebu mbali walifurika katika makanisa mbali mbali kusherehekea siku kuu ya Krismasi.
Hata hivyo, mjini Nairobi, Wakenya wengi ambao walitaka kusafiri kujiunga na jamaa zao katika sehemu za mashambani, wamekwama katika vituo mbali mbali vya basi kutokana na ukosefu na mabasi ya kutosha na pia kupandishwa kwa nauli.
Kampuni nyingi za mabasi zimeongeza nauli kutokana na idadi kubwa ya abiria.