Thursday, June 13, 2013

Kidato cha sita 2013 wanatakiwa kuripoti JKT 24/06/2013

Kidato cha sita 2013 wanatakiwa kuripoti JKT 24/06/2013

TANGAZO


MKUU WA JKT MEJA JENERALI RAPHAEL MUHUGA ANAWAITA VIJANA 10,849 WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA MWAKA 2013 KUJIUNGA NA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA KAMA IFUATAVYO:-

1. VIJANA WOTE WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA WALIOPATA DIVISION I NA DIVISION II.

2. VIJANA WOTE WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA WALIOSOMA MASOMO YA MCHEPUO WA SAYANSI NA KUPATA DIVISION III.

3. VIJANA HAO WANATAKIWA KURIPOTI KATIKA MAKAMBI YA JKT TAREHE 24 JUNI 2013 BILA KUKOSA. AMBAYE HATARIPOTI ATACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA.

4. TANGAZO HILI HALIWAHUSU VIJANA WOTE WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA 2013 KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA UNGUJA NA PEMBA. AIDHA, SHULE 27 AMBAZO VIJANA WAKE WAMEHITIMU MAFUNZO YA JKT AWAMU YA KWANZA HAZIHUSIKI.

5. VIJANA HAO WATUNZE TIKETI ZAO KWA AJILI YA KUREJESHEWA NAULI WATAKAZOTUMIA MARA TU WATAKAPORIPOTI VIKOSINI.

6. TAARIFA ZAIDI ZITATOLEWA KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI YA HAPA NCHINI.

============================== =====

Selections hizi hapa:
Endepo tovuti ya JKT itakuwa ngumu kufunguka, angalia hizi attachments from JF


============================== =====

Kwa maelezo zaidi ya kambi mbali mbali walikopangwa angalia Jeshi la Kujenga Taifa
Attached Files

KENYA NA MALAWI ZATOKA SARE YA 2-2


Late own goal sees Malawi heldTimu za Taifa za Malawi na Kenya zimetoka sare kwa kufungana mabao 2-2 mjini Blantyre katika  mechi ya kufuzu kombe la dunia.

Malawi ndio walikuwa wanaongoza kwa mabao 2-1 lakini katika dakika ya mwisho Chimango Kayira alijifunga na kupunguza  uwezekano wa Malawi kusonga hatua inayofuata.

The Flames ndio waliowa kuwa wa kwanza kupata  bao katika  dakika ya 46, bao lililofungwa na Robion Ngalande, lakini dakika sita baadaye Mohamed Jamal akaisawazishia Harambee Stars.

Katika dakika ya 81, Robert Ng'ambi alifunga bao la pili kwa Malawi, kabla ya Kayira kujifunga na mechi kumalizikia mabao mawili kwa mawili.Matokeo hayo yana maana kwamba mabingwa wa Afrika Nigeria ndio watakaofuzu hatua inayofuata kutoka kundi F, ikiwa wataishinda Namibia mjini Windhoek, mechi inayochezwa baadaye usiku huu.

Hadi kufika leo kumebakia mwaka mmoja, kabla ya fainali za kombe la dunia za mwaka 2014 kuanza nchini Brazil.

LIONEL MESSI NA BABA YAKE WAINGIA MATATANI

 



Mshambulizi wa Barcelona Lionel Messi na babake wanachunguzwa nchini Hispania kwa kuilaghai serikali ya nchi hiyo zaidi ya pauni milioni tatu nukta nne.

Mchezaji huyo kutoka Argentina na babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu zisizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009.Hata hivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hajasema lolote kuhusiana na madai hayo.


Messi hulipwa Euro milioni kumi na sita kila mwaka na ndiye mchezaji anayelipwa kiasi cha juu zaidi duniani.Lakini mwendesha mashtaka Raquel Amado, aliwasilisha nyaraka za mahakama nyumbani kwake kwa mchezaji huyo katika mtaa wa kifahari wa Gava mjini Barcelona.

Jaji mjini humo ni sharti waidhinisha malalamishi dhidi ya mshukiwa yeyote kabla hajafunguliwa mashtaka.Messi na babake wanashukiwa kutumia kampuni katika mataifa ya ngambo, mjini Belize na Uruguay kuuza haki za kutumia picha ya mchezaji huyo.

Mchezaji huyo na babake wanatuhumiwa kutumia kampuni hizo zilizoko nje ya Hispania, ambako anaishi na kucheza soka ya kulipwa, kukwepa kulipa kodi inayokisiwa kuwa pauni milioni tatu na nusu.



WASHINDI WA TUZO ZA KILIMANJARO KUFANYA MATAMASHA MIKOANI


Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa Kili Music Tour 2013 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kala Jeramiah na Nasssib Abdul 'Diamond'. 
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Nassib Abdul 'Diamond' akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya wasanii kwenye mikoa 8, ambapo jumla ya wasanii 24 watashiriki. 
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Kala Jeramiah akizungumzia ziara ya wasanii.
 Chazi Baba akitoa vionjo vya moja ya nyimbo zake. 
 Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe akiteta jambo na, Diamond na Chaz Baba wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu Kili Music Tour 2013.
Profesa J akiwashukuru wale wote waliompigia kura pamoja na kuwasihi wasanii tutokata tamaa na kujipanga vizuri katika tuzo za mwakani ili waje kung'ara. 

TIMU ZA BUNGE ZAPOKEA VIFAA TOKA KWA WAPINZANI WAO TIMU YA NMB

Timu ya Benki ya NMB ipo kwenye maandalizi makubwa ya mechi kati yao na wabunge ambayo itachezwa siku ya jumamosi kwenye viwanja vya Jamhuri  hapa Dodoma. Ili kufanikisha mtanange huo Benki ya NMB imekabidhi jezi kwa Nahodha wa timu ya Bunge ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Kassim Majaliwa. Ni mtanange wa kukata na shoka ambao umesubiriwa kwa hamu na kwa muda mrefu na mashabiki wa timu hizo mbili.

 Mheshimiwa Kassim Majaliwa akipokea jezi kwa ajili ya mechi hiyo kati ya Wabunge na NMB  kutoka kwa Nahodha msaidizi wa timu ya NMB, Hezbon Mpate. Makabidhiano haya ya Jezi zenye thamani ya shilingi milioni tatu na laki saba yamefanyika katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.


Mheshimiwa Fatma Mikidadi akipokea jezi za mpira wa pete kutoka kwa nahodha wa timu ya mpira wa pete ya NMB Josephine Kulwa. Mechi zote zinatarajiwa kuchezwa siku ya jumamosi katika viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma.
 Waheshimiwa wabunge pamoja na maofisa wa NMB wakizifurahia jezi mara baada ya makabidhiano rasmi.

MASCHERANO AONYESHWA KADI NYEKUNDU KA KUMPIGA MTU WA HUDUMA YA KWANZA

Javier Mascherano of Argentina is carried off


Javier Mascherano ameomba radhi kwa kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumpiga mwendesha gari ya kutolea majeruhi kiwanjani katika mchezo wa kufuzu kombe la dunia dhidi ya Ecuador.

Kiungo huyo wa  Barcelona, ambaye aliwahi kuchezea  Liverpool na West Ham, alitolewa baada ya kumpiga dereva wa gari ya kuondolea wachezaji majeruhi kiwanjani katika dakika ya 87.

Mascherano, ambaye alikuwa nahodha wa timu hiyo kwa usiku huo, baadae alisema kuwa: 'Hakuna mtu anayependa fujo nchini kwetu nilifanya makosa  naona  aibu kwa kufanya vile .
mwendesha gari alikuwa anakwenda kwa kasi kubwa sana ilikuwa bado kidogo nidondoke.Nilimkanya (Dereva) lakini alidharau, lakini nilichofanya hakikuwa kitendo  cha kiungwana.‘Ninaelewa umuhimu wa mimi kuomba radhi na nimefedheheshwa na kwa masikitiko nimeomba radhi.’

Kwenye mtandao wa Twitter,: 'Nakiri nimefanya kitendo kibaya, hakielezeki.Baada ya kuumia , mwendesha gari alikuja kunichukua kama sheria inavyotaka japokuwa kiungo huyo, alianzisha fujo kama alivyokuwa akionekana kwenye Tv .na picha za runinga zilionyesha , Mascherano akiwa anapiga makelele kwa wahudumu wa huduma ya kwanza .

ORIGINO KOMEDI YAINGIA MKATABA MNONO NA KAMPUNI YA NEXUS



IMG_7080
Mkuu wa Kitengo cha Vipaji na Uendelezaji wa Biashara wa Kampuni ya Rockstar 4000 Bi. Christine Mosha “Seven” akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo ambapo amesema amefurahishwa sana kufanya kazi na Orijino Komedi ambao ni watu wenye vipaji vya hali ya juu na kuingia mkataba na Kampuni ya Nexus Consulting Agency ambapo kwa pamoja wamedhamiria kukuza na kubadilisha dhama ya vipaji na sanaa kutoka ilipo na kuwa ya kimataifa. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Nexus Agency Bw. Bobby Bharwani na kulia ni Muandaaji wa vipindi vya Orijino Komedi Sekioni David.
IMG_7083
Mkurugenzi Mkuu wa Nexus Consulting Agency Bw. Bobby Bharwani (kushoto) akieleza kuwa kwa upande wa kampuni yao kushirikiana na Orijino Komedi ni kitu muhimu kwa Nexus kwani siku zote imekuwa ikitamani kufanya kazi kwa karibu na kundi hilo na kuthamini kazi zao kutokana na vipaji vya hali ya juu walivyokuwa wakionyesha wasanii wa kundi hilo.
IMG_7051
Picha ya pamoja kati viongozi wa makampuni ya ‘Nexus Consulting Agency’ na ‘Rockstar 4000′ na wasanii wa kundi la Orijino Komedi mara baada ya kutolewa kwa taarifa ya kundi hilo kuingia mkataba na makampuni hayo.
Kundi la kipaji cha Televisioni “Orijino Komedi” linaloongoza nchini kwa vipindi vyake kupitia televisionilimeingia mkataba na Kampuni ya Nexus Consulting Agency kwa kushirikiana na Rockstar 4000, ambao utakuwa ni mkataba wa kwanza kwa wasanii wa luninga kupitia kampuni ya Nexus.
Nexus imenunua haki zote za usimamizi wa biashara na uongozi wa kundi hilo ambalo linajulikana sana nchini kupitia vichekesho vyake vinavyoonyeshwa na vituo vya television na matamasha mbalimbali, ambapo mkataba huo utakuwa ni kwa ajili ya kusimamia kipindi hicho cha vichekesho kinachoundwa na wachekeshaji saba ambao ni Joti, Macreagan, Masanja, Wakuvanga, Mpoki, Vengu na Seki David ambacho kimekuwa hewani kwa mfululizo wa miaka sita.
Kwa kushirikiana na Rockstar 4000, Nexus imesema itahakikisha inaendeleza vipaji vya wasanii wa kundi hilo ili vipaji vyao viweze kufikia kiwango cha juu cha ufanisi ndani ya Afrika na Kimataifa kwa ujumla.

KIINGILIO MECHI YA STARS, IVORY COAST 5,000/-

Kiingilio cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Ivory Coast (The Elephants) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.
Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.
Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.
Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku mbili kabla ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.
Utaratibu katika mechi hiyo utakuwa kama ilivyokuwa katika mchezo wa Simba na Yanga, ambapo hayataruhusiwa kuingia uwanjani isipokuwa kwa yale yatakayokuwa na sticker maalumu kutoka TFF.

Tuesday, June 11, 2013

GARI AINA YA CENTER YAUA MWANAMKE BAADA YA KUSHINDWA KUPANDA MLIMA NA KUPINDUKA MORO


 Askari wa jeshi la polisi wakiandika maelezo ya awali mara baada ya mchoro, kufuatia gari aina ya center kupata ajali na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia papo hap
o baada ya kupinduka ambapo chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa ni kushindwa kupanda mlima katika barabara ya mjini-Forest Hill eneo la shule ya msingi Mlimani mkoani Morogoro.
 Chini mwili wa marehemu ukiwa katika mtaro
 Wasamalia wema wakipakiza maiti katika gari ya polisi kwa ajili kwenda kuhifadhi katika chumba cha maiti hospitali ya mkoa wa Morogoro
 Hapa magunia yenye mpunga yakiwa wameanguka kutoka kwenye gari hilo.
 Huyu ni mume wa marehemu akiwa eneo la tuko baada ya kupata taarifa za ajali hiyo.
 Gari la polisi ambalo lilibeba maiti kabla ya kuondoka eneo la tukio
 Mwili wa marehemu ukiwa umepakiwa katika gari hilo la polisi

AJALI MBAYA YATOKEA CHUMA ROAD, MWENDESHA BODABODA AFARIKI PAPO HAPO. TAZAMA PICHA

Ajali imetoke Mtaa wa chuma road karibu na bodi ya nafaka! Na Simba plastiki
 Wenye pikipiki walikua wanatoka Veta kunyoosha mbozi roar na mwenye gari anatokea kwa sokota, mwenye gari akapinda kona ya Simba Plastiki na kuwazoa wenye pikipiki,na asilimia mia dereva kafanya dharau saaana,maana alipinda gari ikiwa kwenye speed kubwa sana






TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Sunday, June 9, 2013

HII NDIYO MAKALA ILIYOCHAMBULIWA JUU YA FREEMASON NA HISTORIA YAO HII HAPA.


HISTORIA FUPI YA FREEMASON.
ni shirika ambalo mambo yake ni siri kuu. Mimi nilifanya utafiki kwenye mitandao, nikafatilia historia yao kama inavyoonyeshwa mara kwa mara kwenye makala za historia katika televisheni za magharibi pamoja na kuongea na watu waliofuatilia kwa karibu mambo yao.
Kwenye maelezo yao kwa nje Free masons wanajitangaza kama shirika zuri tu.
Naomba niorodheshe mambo machach

e niliyoambiwa kuhusiana na Freemasonry.
1. Ni kweli Freemasonry kama ilivyo maana yake kwanza ilkuwa ni kundi la mafundi waashi (masons) au wajenzi kuwa lugha nyingine. Walikuwa ni wataalamu waliobobea kwenye masuala ya ujenzi wa mahekalu na mabenki ya zama hizo zinazoitwa kwa kizungu (medieval times).

Niliambiwa walikuwa ni watunzaji wa pesa za kanisa katoliki. Kwani walikuwa wanajenga mahekalu(cathedrals) za wakatoliki na mabenki/ mahandaki ya kuhifadhia pesa pamoja na kuzikia(catacombs).

Niliambiwa wanaweza kujenga hayo maandaki kwa utaalamu mkubwa kiasi kwamba ukiingia ndani ya hayo mahandaki bila ramani unaweza ukashindwa kutoka hata unaweza kupotelea humo humo ndani usiweze kutoka tena. Hicho ndicho kilichokuwa ni kiwango cha utaalamu wao.

2. Kwa kuwa walikuwa ni waashi ndiyo maana alama zao ni vifaa vya ujenzi, Pima maji n.k

3. Inasemekana mji mkuu wa marekani (Washington DC) ulisanifiwa na kujengwa na Freemasons. Na inasemekana ni mji makini ambao umejengwa ukizingatia pembe tatu zenye nyuzi zinazowakilisha u freemason.

3. Ikatokea kipindi ambapo hawa freemasons wakaasi kwa kuanza kujishirikisha na mambo ya nguvu za giza. Wengine wanasema walianza kuiba pesa za kanisa katoliki, lakini ukweli halisi haujulikani. Kutokana na sababu hizi na zinginezo ambazo ni siri kati ya kanisa katoliki na freemasons, Freemasons wakafukuzwa kutoka ukatoliki.

Ndio maana hakuna maelewano kati ya freemasons na wakatoliki. Wakatoliki wakaanzisha shirika jingine badala ya hao freemasons lijulikanalo kama Jesuits.

Jesuit Fathers ni mapadri wa katoliki wa daraja la juu sana wenye elimu ya juu zaidi ambao hufanya kazi za siri za utawala na udhibiti ndani ya kanisa katoliki.

4.Kuhusu imani yao (freemasons) nikaelezwa kwa kifupi kuwa wanaamini Yesu na Lucifer ni mtu na ndugu yake. wanaamini kuwa Lucifer ndiye mwema na mzuri lakini wanaamini kuwa Yesu ndiye mwenye mabaya. alimfanyia hila Lucifer aonekane mbaya.

4.Kinachoendelea ndani yake kuhusiana na ibada zake ni siri kwani kuna daraja ambazo muumini wa freemason anapanda kutokana na kubobea katika imani ikiwa ni pamoja na kutunza siri zao. Ninajua kuwa daraja ya juu kabisa ni nyuzi ya 33 (33rd degree)

5. Ni watu wenye nguvu mno na mambo yao ni makubwa mno na siri zao ni nzito mno. Ndiyo maana haziko wazi.

Wafuasi wa kiwango cha chini wala hawajui shirika hili linahusika na nini manake hata wao hawaambiwi kitu. Kwa wafuasi wa daraja ya chini wanakwenda ku socialize tu. Yaani kwa wasio jua kitu kule kwenye lodge zao ni kama ywca au wmca au club hivi. Kwenye nchi kama marekani watu wasio jua siri wanachukulia kama sehemu za kusocialize tu.

6. Freemasonry inawekwa pamoja na makundi mengine makubwa ya siri, yanayoendesha ulimwengu mzima kwa nguvu za kiuchumi, siasa na mambo ya utawala.



WALIOSHIRIKI KUPINGA FREEMASON NA UASI WA LIONS CLUB NA ROTERY CLUB
Kanisa la Katholiki wakati moja waliwahusisha Rotarians (Lions Club) moja kwa moja na Freemasons. Mwaka wa 1928 Maaskofu wa kihispania walitangaza wazi kwamba Rotary Club si chama tu cha kawaida bali ni Muungano au chama kipya cha kuabudu mashetani wakiwa na katiba, tabia na kila kitu chao kufanana na zile za Freemasons wakawatahadharisha waumini wao wajichunge sana na Chama hicho, na baada ya muda mfupi wakuu wa Vatican walitoa amri kwamba maaskofu wa kanisa la katoliki hawaruhusiwi kujiunga na vyama hivyo (Rotary, Lions Club).

Mohammed Sayed Tantawi
Katika miaka ya 1970 kiongozi wa juu na Sheikh wa Chuo kikuu cha kiisilamu huko Misri (Egypt) inasemekana alitoa fatwa kuwakataza waisilamu wasijiunge na chama cha Rotary Club na wakati mambo haya yalikua yakikatazwa na dhehebu la sunni Chama cha rotary pia kilisikika kukatazwa na Ayatollah Khomeini.

Ayatollah Khomeini
katika mwaka wa 1798 Mwandishi Mmoja wa Kiingereza aliejulikana kwa jina la john Robbinson aliandika kitabu kijulikanacho kama Proofs of a Conspiracy Against All the Religions and Governments of Europe, Carried On in the Secret Meetings of Free Masons, Illuminati, and Reading Societies (Uthibitisho wa njama dhidi ya Dini zote na Serikali zote za Ulaya ilipangwa katika mikutano ya siri ya Freemasons, Illuminati, na vyama vinginevyo vya Reading)

John Robbinson
Kitabu hicho kinaelezea Ari na hamasa za Freemason walivyokuwa wakipanga kisiri jinsi ya kupinduwa mipangilio mizuri ya Maisha (Serikali) na ndio waliosababisha mapinduzi nchini Marekani na Ufaransa.

Shuku za kuenea kwa Freemasons zilienea hadi kufikia miaka ya 1800 ambapo
Rais Wa 13 Millard Fillmore wa Marekani
alichaguliwa kwa mara ya kwanza katika bunge la Marekani (Congress) kama mgombea aliyekuwa akipinga mambo ya Freemasons na akafikia kilele katika karne ya 20 (20th Century)

Sergiei Nilus Mwandishi Kitabu cha Protocol
Kitabu cha The Protocols of the Elders of Zion sio kuhusu mayahudi kutawala dunia lakini ni kuhusu njama za freemason wa kiyahudi kubadili mfumo wa dunia.

Hitler Reinhard Heydrich
Hitler alizungumzia kuhusu njama za Mayahudi-Bolshevik-Freemason na kiongozi mwingine wa Ujerumani kwa jina la Reinhard Heydrich aliunda kikosi maalum (Special Section SS) kuangamiza ushawishi wa freemason nchini Ujerumani.

Moqtada al-Sadr Al Hawza
Nchini Irak, Gazeti la Moqtada al-Sadr lijulikanalo kama Al Hawza lilichapisha picha ya George H.W. Bush na Bill Clinton na akaelezea kwamba ishara ya mikono yao ilikuwa ni alama ya waandamizi wa kizayoni na freemason, na kama walivyo Wakatoliki Waisilamu pia waliwahusisha wanchama wa Rotary moja kwa moja na Freemasons na kusema vyama vyote viwili ni laana.

Rais Bush Rais Clinton
Freemasons wamehusika moja kwa moja katika jitihada za kutawala Mashariki ya kati jitahada ambazo zilibuni uhasama kati ya Mashariki ya Kati na Jumuiya ya Magharibi.
Freemason walitoa fursa ya wafanyabiashara kuunda mtandao mmoja, hii ni katika malengo ya wafanyabiashara wanachama wa Freemason wa Ulaya wafungue ofisi za Freemason nje ya nchi na kuwaalika wanainchi wa Ulaya kujiunga nao.

Kwa ujumla sio Wafanya biashara wa Wakiingereza au Mashariki ya kati ndio waliowengi tu kama anavyoeleza bwana Hamid Algar wa Berkeley ambaye ni Mwanachuoni maarufu duniani wa historia ya Kiisilamu:-

Hamid Algar
Freemason imeweza kuhudumika katika uisilamu tangu kijitambulisha kwa waisilamu katika karne ya 18 kama njia ya kukuza utawala wa fikra za wa Magharibi kisiasa na kimawazo; Mojawapo wa Ofisi za Freemason huko Istambul nchini Uturuki, ilikuwa na Balozi wa Uingereza kama mkuu

LIST YA WATU MAARUFU AMBAO NI WANACHAMA KWA MWAKA 2013

  • Jay Z
  • Dr DRE
  • Cypress Hill
  • Chris Brown
  • Drake
  • Celine Dion
  • Halley Berry
  • Eminem
  • Rick Ross
  • TB Joshua
  • Charlie Boy
  • Tonto Dikeh
  • Davido
  • Wizkid
  • P-Square Twins
  • Britney Spears
  • Aaliyah
  • Nicki Minaj
  • Beyonce Knowles
  • Alicia Keys
  • David Bowie
  • Madonna
  • Paris Hilton
  • Barack Obama
  • Aretha Franklin
  • Bob Marley
  • Angelina Jolie
  • Jim Carey
  • Bob Dylan
  • David Bowie
  • Late Michael aliuliwa baada ya kuwageuka
  • Justin Bieber
  • Kanye west
  • Marilyn Manson
  • Lady gaga
  • Lil Wayne
  • Late Tupac Sharkur aliuliwa baada ya kuwageuka
  • Nas
  • Rihanna
  • P-Diddy
  • Wiz Khalifa
  • Late Whitney Houston aliuliwa baada ya kuwageuka
  • T-pain
  • Rihanna
  • Kim Kardashian

  • William F. Buckley, Jr.
  • George H. W. Bush
  • George W. Bush
  • Bill Clinton
  • Hillary Rodham Clinton
  • Al Gore
  • Gerald Ford
  • Ronald Reagan
  • Richard Nixon
  • Lyndon B. Johnson
  • John F. Kennedy
  • Ted Kennedy
  • Henry Kissinger
  • Mikhail Gorbachev
  • Guy de Rothschild
  • John D. Rockefeller
  • Mary Astor
  • Clifford Dupont
  • Andrew W. Mellon
  • Dick Cheney
  • Robert Colin Boyd
  • Kris Kristofferson
  • Boxcar Willie
  • Bob Hope
  • Elizabeth II, Queen of Great Britain
  • Prince Philip, Duke of Edinburgh
  • Charles, Prince of Wales
  • Prince Andrew, Duke of York
  • Princess Anne, Duchess of Calabria
  • Winston Churchill
  • Franklin D. Roosevelt
  • Joseph Stalin
  • Adolf Hitler
  • Bill Gates
  • Barrack Obama
  • Alan Greenspan
  • Ben Bernanke


FREEMASON IN TANZANIA

Tanzania ina wanachama hai zaidi ya 600 wa kundi la watu wenye imani ya siri ya Freemasons wakiwa wanatokana na watu wa kada mbalimbali wakiwemo maarufu, huku ikielezwa kwamba miongoni mwao hakuna viongozi wakuu wa serikali.

Hayo yalibainishwa na Kiongozi wa kundi la Freemasons katika eneo la Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Sir Andy Chande alipozungumza na gazeti hili (HabariLeo), wiki hii Dar es Salaam.

Kiongozi huyo Mtanzania mkazi wa Dar es Salaam mwenye asili ya Kiasia, alisema licha ya Tanzania kuwa na wanachama hao, kwa sasa idadi ya wanachama duniani inapungua tofauti na inavyoonekana sasa kuwa wanaongezeka kutokana na kuibuka maneno mengi kuhusu kundi hilo.

Alisisitiza kuwa si rahisi kumjua mwanachama wa kundi hilo, bali wenyewe ndio wanaofahamiana, akisema ni siri na kwamba wenyewe wanakutana katika vikao mbalimbali mara moja kwa mwezi au zaidi.

Alisema nchini kuna wanachama wakiwemo wafanyabiashara, watumishi serikalini, walimu pamoja na wanataaluma mbalimbali wanaoheshimika sana na kusisitiza kuwa kuna maneno mengi yanayosemwa kuhusu kundi hilo, ambayo siyo ya kweli. Alisema idadi ya wanachama wake duniani inazidi kupungua kutoka milioni nane hadi sasa wako milioni sita, tofauti na wengi wanaodhani kuwa idadi hiyo inaongezeka.

Chande alizungumza na mwandishi wa habari hizi katika Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert ambako yeye ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule alipozungumzia maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, alisema duniani kuna watu wazito wengi ambao ni wanachama wa kundi hilo kama majaji wakubwa na hata Binamu wa Malkia Elizabeth wa Uingereza ni kiongozi mkubwa wa kundi hilo.

Akizungumzia masharti ya kujiunga na kundi hilo, Chande alisema ni lazima mwanachama huyo awe anaamini katika Mungu bila kubagua iwapo ni Mkristo au Muislamu.

Alisema pia ni lazima anayetaka kujiunga awe na umri unaozidi miaka 21 na walio chini ya umri huo hawaruhusiwi kujiunga na lazima familia ya anayetaka kujiunga na wanandugu wafahamu kuwa umejiunga na kundi hilo.

“Unajua katika imani hii kuna michango mbalimbali ambayo unatakiwa kutoa ambayo ni zaidi ya dola milioni sita (karibu Sh bilioni 10), hivyo ni lazima ndugu wafahamu ili kuepuka matatizo utakapotakiwa kutoa,” alisisitiza.

Alisema si kweli kuwa wenye fedha wengi ni wanachama wa kundi hilo huku akikanusha wanachama wanajiunga kwa ajili ya kupata fedha, bali ni dini kama imani nyingine. Alisisitiza kuwa hakuna ukweli kwamba wanaopata mafanikio katika maisha wakiwa ndani ya imani ya Freemasons kuwa wanatoa kafara watu wao wa karibu kwa lengo la kupata utajiri.

Chande pia alisema hairuhusiwi kutumia jina la kundi hilo kwa nia ya kujipatia nafasi sehemu mbalimbali au kuongeza nafasi katika chuo au shule.

BAADA YA KUJIUNGA: Pia unatakiwa kujifunza vitu vingi na kuvihifadhi kichwani kama vile maneno ya kusema wakati unafanya ibada za freemasons kwa sababu tukiwa pamoja tunavyozungumzia sifa za kuwa binadamu kamili unaweza ukafananisha na ibada ya kanisani. 

CHANZO http://nyumbayahabari.blogspot.com

FREEMASON UKUMBI WA KWANZA KUTUMIWA NA BUNGE LA TANZANIA 


 

 Ukumbi wa Freemason, Dar es Salaam




 

 Ukumbi wa Arnatouglou, Dar es Salaam

 

 Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam





 Ukumbi wa Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi, Dodoma



 Ukumbi wa Pius Msekwa, Dodoma



Watu wengi wamekuwa wakitafuta namna ya kujiunga na ufreemason kama ulikuwa hujui hawa ndo watanzania ambao wamekuwa wakikesha kutafuta nafasi ya kujiunga na ufreemason




UNAAMBIWA HIZI NDIZO ALAMA ZA MAFREEMASON





















 NAHIZI NDIZO ISHARA ZAO





 WASANII MAARUFU WANAOJIHUSISHA NA UFREEMASON