Friday, April 26, 2013

Rais mpya wa Kenya akipokezwa mamlaka


Waandamana kuhusu Korosho Tanzania

Takriban nyumba 20 zimeteketezwa katika maandamano yaliyofanywa na wakulima wa Korosho pamoja na waandamanaji wengine Kusini mwa Tanzania.
Hii ni kwa mujibu wa mbunge mmoja wa eneo hilo.
Mbunge huyo, Faith Mitambo alisema kuwa majengo mawili nyumbani kwake mjini Liwale, yalichomwa na kuwa nyumba zingine mali ya baadhi ya wanachama wa chama tawala CCM ziliteketezwa.
Uharibifu huo ulianza baada ya wakulima kulipwa kiasi kidogo cha pesa ikilinganishwa na zile walizokuwa wamekubaliana kulipwa na serikali baada ya kuiuzia mazao yao mwaka jana.
Polisi zaidi wamepelekwa katika eneo hilo kuzuia ghasia zaidi.
Bi Mitambo, aliyekuwa mjini, Dodoma, wakati huo aliambia BBC kuwa alikuwa anazuru eneo bunge lake kudadisi hali ilivyo.
Alipokea habari kuwa waandamanaji waliokuwa wanajumuisha vijana , walianza kufanya fujo vijijini mnamo Jumanne asubuhi hadi walipofika mjini Liwale saa za jioni.
Mkaazi mmoja wa mji huo aliambia BBC kuwa mnamo Jumatano kulikuwa na hali ya wasiwasi mjini humo na kwamba polisi walikuwa wamewarushia gesi ya kutoa machozi wandamanaji ili kuwatawanya.
Maelfu ya wakulima wadogo wadogo wanaopanda Korosho nchini Tanzania na ambao huvuna mazao yao mwezi Oktoba, huyauza kwa mashirika mbali mbali kwa bei waliyokubaliana.
Mwandishi wa BBC mjini Dar es Salaam, Erick Nampesya anasema kuwa wakulima walikubaliana kulipwa shilingi 1,200 pesa za Tanzania kwa kila kilo ya korosho hizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, wakulima walilipwa sehemu ya deni lao.
Lakini pale waakilishi kutoka kwa mashirika walipokwenda katika wilaya ya Liwale, kuwalipa sehemu ya mwisho ya deni lao, wakawa wamebadilisha makubaliano waliyokuwa wameafikiana.
Wakulima walilipwa nusu au chini ya nusu ya deni lililokuwa limesalia, baada ya kuambiwa kuwa bei ya Korosho ilikuwa imeshuka sana katika soko la kimataifa.
Wanasiasa wakuu ambao wakulima hao wanawalaumu kwa kukosa kuwasaidia ndio walikuwa wamewaelekezea ghadbabu zao
Wakulima wamekuwa wakilalamika kuhusu msukosuko wa bei za Korosho ambayo huathiriwa zaidi kulingana na msimu.

Mshukiwa wa mauaji Darfur auawa Sudan

Mmoja wa waasi wa Sudan anayeshtakiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, kwa makosa ya uhalifu wa kivita katika jimbo la Darfur ameuawa, kwa mujibu wa jopo la mawakili wake wa utetezi.
Taarifa zinasema, Saleh Mohammed Jerbo Jamus alifariki dunia Ijumaa iliyopita mchana wakati wa mapigano huko Darfur Kaskazini.
Alitarajiwa kufikishwa mahakamani Mei 2014, kujibu mashtaka ya kuhusika na shambulio baya dhidi ya vikosi vya kulinda amani vya Afrika vilivyokuwa Darfur mnamo mwaka 2007.
Mwandishi wa BBC mjini The Hague, Uholanzi anasema lazima mahakama hiyo ipate uthibitisho kuhusu kifo hicho kabla ya kuifuta kesi.
Jerbo na kiongozi mwenzake wa waasi wa Darfur, Abdallah Banda Abakaer Nourain wanakabiliwa na mashtaka matatu ya uhalifu wa kivita yanayohusishwa na mauaji ya askari 12 wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika katika shambulio lililofanyika katika kambi ya askari hao ya Haskanita Septemba 2007.
Jerbo aliuawa wakati wa shambulio kwenye makazi yake lililofanywa na wapiganaji wa kundi lililojitenga kutoka kundi la Justice and Equality Movement linaloongozwa na Gibril Ibrahim.
Watu hao wawili walijisalimisha kwa hiari katika mahakama ya ICC mwaka 2010 ili kukabili mashtaka, na walikua huru kuondoka Uholanzi na kurudi mahakamani pale walipohitajika.
Kwa mujibu wa ICC, Jerbo alikuwa ni Mnadhimu Mkuu wa kundi la waasi la SLA – Unity, wakati wa shambulio la mwaka 2007, lakini sasa alikuwa kwenye kundi la Justice and Equality Movement.
Rais wa Sudan, Hassan Omar Al Bashir, mawaziri wake wawili na kiongozi mmoja wa kundi la wanamgambo linaloiunga mkono serikali pia wameshtakiwa na mahakama ya ICC kwa uhalifu wa kivita Darfur lakini mpaka sasa hawajakamatwa.
Wote wamekanusha mashtaka dhidi yao wakidai kwamba, machafuko ya Darfur yametiwa chumvi kwa sababu za kisiasa.
Mzozo wa Darfur ulianza miaka 10 iliyopita baada ya waasi kuanza kushambulia maeneo ya serikali, wakiishutumu Khartoum kwa kuwakandamiza Waafrika na kuipendelea jamii ya Kiarabu.
Kundi la wanamgambo wa Kiarabu la Janjaweed, wakati huo lilishutumiwa kwa kuendesha mauaji ya kikabila dhidi ya raia Waafrika wa Darfur.
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, inakadiriwa kwamba, zaidi ya watu 300,000 walipoteza maisha kutokana na mzozo wa Darfur. Lakini serikali ya Khartoum inaweka idadi hiyo kuwa ni watu 12,000.
Watu wengine zaidi ya milioni 1.4 wameachwa bila makaazi. Ingawa machafuko ya Darfur yamepungua sana bado kuna mapigano kati ya vikosi vya serikali, waasi, na vikundi vinavyotofautiana kikabila.

Generali wa Brazil kuongoza kikosi DRC

Umoja wa Mataifa umemteua Generali mmoja raia wa Brazil ambaye anasifika kwa kudhibiti mtaa mmoja wa mabanda nchini Haiti kutokanamana na vurugu kuweza kuwaongoza walinda amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Generali Carlos Alberto dos Santos Cruz ataongoza kikosi cha wanajeshi 20,000, ikiwemo kikosi kipya cha wanajeshi kitakachopambana na waasi mashariki mwa nchi.
Hii ndio mara ya kwanza kwa Umoja wa mataifa kukabidhi kikosi cha wanajeshi nguvu kuweza kupambana na waasi.
Generali Santos Cruz, aliambia BBC kuwa wanajeshi wake, watafunzwa namna watakavyo pambana na waasi bila kuwajeruhi raia na kuharibu mali nchini Congo.
"eneo tete zaidi siku hizi ni Mashariki mwa nchi,'' Cruz alimbia BBC
"niko tayari kukabiliana, na hali ngumu zaidi. Lengo kuu ni kuwaondolea hali ngumu wanayokabiliana nayo watu wa Congo.''
Generali Santos Cruz ataongoza kikosi cha wanajeshi 2,500, wakiwa na jukumu la kuwapokonya silaha waasi pamoja na kuwarejesha katika maisha ya kiraia Mashariki mwa DR Congo.''
Kikosi cha walinda amani cha Umoja wa mataifa,kilichoko Congo kimekosolewa sana kwa kukosa kumaliza vita, vya miongo miwili.
Wanajeshi kutoka Tanzania, Malawi, Msumbiji na Afrika Kusini ndio walio wengi katika kikosi hicho na wataanza kazi yao mwezi Julai.
Generali Santos Cruz ni kamanda mstaafu, wa kikosi kilichowahi kutumwa nchini Haiti, na anasifiwa kwa kupambana vikali na megenge ya majambazi nchini Humo mwaka 2007

UN kupigia kura azimio kuhusu Mali


Baadhi ya wanjeshi wa Chad walio nchini humo pia wataanza kundoka
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupigia kura azimio linalopendekeza kuundwa kwa kikosi cha kulinda amani nchini Mali.
Kikosi hicho chenye wanajeshi 12,600 kinajumuisha takriban wanajeshi 6,000 kutoka nchi za Magharibi mwa Afrika ambazo tayari zina wanajeshi wao nchini humo.
Azimio hilo limependekezwa na Ufaransa ambayo iliingilia kati mzozo wa Mali mnamo mwezi Januari ili kupambana na wapiganaji wa kiisilamu Kaskazini mwa nchi hiyo.
Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Mali mwanzoni mwa mwezi Julai kabla ya uchaguzi mkuu.

Hata hivyo duru zinasema kuwa azimio hilo limezua mjadala mkali.

Makundi ya kiisilamu yaliweza kutumia pengo la usalama lililotokea baada ya mapinduzi ya kijeshi mwaka jana na kuanza kushinikiza watu kufuata sheria za kiisilamu.
Miji iliyo Kaskazini mwa nchi, imeweza kudhibitiwa na jeshi la Ufaransa lakini baadhi ya wapiganaji wangali katika maficho yao.
Ufaransa ilianza kuondoa baadhi ya wanajeshi wake 4,000 mapema mwezi huu kutoka nchini humo, lakini imekuwa ikishinikiza Umoja wa Mataifa kupeleka wanajeshi wake.
Aidha wanajeshi wa Chad, wanasemekana kuwa wenye uzoefu mkubwa zaidi katika kupambana na wapiganaji jangwani, lakini nchi hiyo pia imeanza kuondoa wanajeshi wake kutoka Mali.
Sababu ya kikosi cha Umoja wa mataifa ni kulinda amani na kitakuwa na wanajeshi 11,200, pamoja na polisi 1,440.
Lengo lake kuu litakuwa kuweka uthibiti katika baadhi ya sehemu za Kaskazini mwa Mali ili kumaliza vitisho kutoka kwa wapiganaji wa kiisilamu.
Hata hivyo rasimu ya azimio hilo haisemi ikiwa wanajeshi hao wataweza kupigana na wapiganaji wa kiisilamu wenye uhusiano na kundi la al-Qaeda, lakini wanajeshi 1,000 wa Ufaransa,wataweza kusalia Mali.

HAYA NDIO MAKUBWA YALIYOANDIKWA NA MAGAZETI YA LEO APRIL 26 2013

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.